Uncategories Picha: Rambo alivyomuibukia Pacquiao Gym
Picha: Rambo alivyomuibukia Pacquiao Gym
Bondia Mfilipino, Manny Pacquiao akiwa na gwiji wa filamu za kibabe Marekani, Sylvester Stallone maarufu kama Rambo au 'Bondia Rocky' mjini Las Vegas, Marekani. Pacquiao yupo katika maandilizi ya mwisho na pambano na Jessie Vargas Novemba 5 mjini Las Vegas uzito wa Welter na mwishoni mwa wiki alitembelewa na Rambo katika gym ya Wild Card mjini Hollywood
Monday, October 31, 2016
Lowassa, Sumaye watua Dodoma
Wakati vikao vya Bunge vikianza kesho mjini Dodoma, Chadema imejipanga kukabiliana na hoja za Serikali ukiwamo muswada wa huduma za vyombo habari utakaojadiliwa kabla ya kupitishwa na kuwa sheria.Tokeo la picha la lowassa na sumaye
Katika vikao hivyo, miongoni mwa miswada itakayojadiliwa ni muswada huo na tayari Waziri wa Habari, Nape Nnauye ameshauwasilisha kwenye Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii ambayo imekamilisha kazi yake jana.
Tayari viongozi wa Chadema akiwamo aliyekuwa mgombea urais wa chama hicho mwaka 2015, Edward Lowassa na Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye wametua mjini humo kupanga mikakati pamoja na wabunge wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), jinsi ya kukabiliana na hoja mbalimbali.
Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema alikiri kuwapo kwa vikao kati ya Lowassa na wabunge wa Ukawa, lengo likiwa ni kuukabili muswada huo.
Alikiba, Diamond, Ommy wakutana kwenye kipengele kimoja Tuzo za ASFA 2016
Waandaaji wa tuzo za mitindo za Uganda, Abryanz Style and Fashion Awards wametangaza majina ya mastaa watakaowania vipengele mbalimbali.
Wakali wa muziki wa Afrika mashariki, Diamond, Alikiba, Ommy Dimpoz na Sauti sol wamekutana kwenye kipengele kimoja cha ‘Most stylish artiste’ Huku Juma Jux, Nedy Music na Idris Sultan wakikutana kwenye ‘Male Most dressed Celebrity’
Jokate Mwegelo, Wema Sepatu na Wolper Stylish watachuana na Vera Sidika, Huddah Monroe na Kate Peyton kweney ‘Female Most dressed Celebrity’
Hii ndio orodha kamili ya Nominees,
FASHION DESIGNER OF THE YEAR
Martin Kadinda (Tanzania)
Sheria Ngowi (Tanzania)
Bobbins & Seif (Uganda)
Moise Turahirwa (Rwanda)
Makeke International (Tanzania)
Jamila Vera Swai (Tanzania)
MOST STYLISH ARTISTE
Males
Sauti Sol (Kenya)
Ali Kiba (Tanzania)
Diamond Platnumz (Tanzania)
Ommy Dimpoz (Tanzania)
Females
Vanessa Mdee (Tanzania)
Avril (Kenya)
Vicotria Kimani (Kenya)
Aika Navy kenzo(Tanzania)
BEST DRESSED CELEBRITY
Males
Nick Mutuma(Kenya)
Juma Jux(Tanzania)
Nedy Music(Tanzania)
Idris Sultan(Tanzania)
Georgie Ndirangu(Rwanda)
Jamal Gaddafi(Kenya)
Females
Jokate Mwegelo(Tanzania)
Vera Sidika(Kenya)
Huddah Monroe(Kenya)
Wema Sepatu(Tanzania)
Kate Peyton (Rwanda)
Wolper Stylish(Tanzania)
MOST FASHIONABLE MUSIC VIDEO
Mamacita – Tinie Tempah ft. Wizkid
Colours of Africa – Diamond Platnumz ft. Mafikizolo
Soft Work – Falz the bahd Guy
Vanessa Mdee – Niroge
No Kissing – Patoranking ft. Sakordie
Aje – Ali Kiba
If I start to talk – Tiwa Savage ft. Dr. SID
Tulale Fofofo – Micasa FT. Sauti Sol
Kontrol – Maleek Berry.
MOST STYLISH COUPLE
Barbie and Bobi Wine (Uganda)
Bonang Matheba & AKA (South Africa)
Annabel Onyango and Marek Fuchs (Kenya)
Zari Tlale and Diamond Platnumz(Tanzania)
Mr & Mrs Ayo Makun(Nigeria)
Elikem and Pokello(Zimbabwe)
CROSSING BOARDERS WITH FASHION
Jidenna
Ugo Mozie
Lupita Nyongo
LOLU ESQ
BEST DRESSED MEDIA PERSONALITY/ENTERTAINERS OF THE YEAR(AFRICA)
Males
Uti Nwachukwu
Falz the bahd Guy
Idris Sultan
Friday James
Ebuka Obi
Derenel Edun
Georgie Ndirangu(Rwanda)
Females
Vimbai Mutinhri
Toke Makinwa
Stephanie Coker
Bolanle Olukanni
Berla Mundi
Bonang Matheba(SouthAfrica)
Tracy Wanjiru(Kenya)
Lissu, Bulaya waingia Kamati Kuu Chadema
Taarifa iliyotolewa jana na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama hicho, Tumaini Makene, ilieleza kuwa katika uchaguzi huo ulifanyika Dodoma jana, uliwachagua Tundu Lissu, Godblesss Lema, Joseph Mbilinyi, Ester Bulaya na Mariam Salum Msabaha kuwa wajumbe wa Kamati Kuu.
Alisema kutokana na Serikali kuamua kupuuza maoni Kamati Kuu ya Chadema katika kikao chake cha kawaida kilichoketi Oktoba 22-23, jijini Dar es Salaam, iliazimia kutuma ujumbe wa baadhi ya wajumbe waandamizi wa Kamati Kuu kwenda Dodoma kukutana na wabunge wa Chadema kujadiliana na kutoa maelekezo ya chama.
Wajumbe walioteuliwa ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Profesa Abdallah Safari, Profesa Mwesiga Baregu, Arcado Ntagazwa na Mawaziri wakuu wa zamani ambao pia ni wajumbe wa Kamati Kuu, Edward Lowassa na Frederick Sumaye.
Saluti ya polisi kwa Lipumba yazua maswali
Askari wa Jeshi la Polisi akimpigia Saluti Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Profesa Ibrahim Lipumba
Suala la polisi kumpigia saluti mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Profesa Ibrahim Lipumba limezua mjadala baada ya kuonekana kuwa si mmoja wa viongozi wanaopaswa kupata heshima hiyo kisheria.
Juzi, Polisi alionekana akimpigia saluti Profesa Lipumba katika eneo la Buguruni alipokwenda kufanya usafi. Kitendo hicho kimeibua mjadala mitandaoni, watu wakihoji uhalali wa mwanasiasa huyo kupewa heshima hiyo.
Juni 2005, aliyekuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Kapteni John Chiligati alipokuwa akijibu swali la aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu, Salome Mbatia alibainisha maana ya saluti na makundi ya watu wanaostahili kupigiwa saluti na askari.
Chiligati alisema saluti ni kitendo kinachofanywa na askari kwa maana ya kutoa salamu kwa ishara yenye kuonyesha heshima. Pia, alisema saluti ni njia mojawapo ya kuonyesha heshima na utii kwa kiongozi mkuu kwenye asasi za kijeshi.
Watunukiwa vyeti kwa kusaka mwili wa marehemu mtoni
VIJANA 15 wilayani Kilolo mkoani Irinbga, wametunukiwa vyeti vya pongezi baada ya kufanikiwa kuupata mwili wa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Lutangilo, Frank Kastiko, aliyefariki dunia hivi karibuni kwa kusombwa na maji ya Mto Lukosi.
Akiwatunuku vyeti vijana hao, Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Asiah Abdallah aliwapongeza kwa kujitolea kutafuta mwili wa marehemu.
“Kutokana na taarifa niliyoipata kuhusu mto na ajali ya mwanafunzi huyo, hakuna shaka kwamba kazi mliyofanya ya kuutafuta mwili wa kijana mwenzenu ilikuwa ngumu na ya uungwana,”alisema.
Mkuu wa shule hiyo, Sebastian Chaula alisema mwanafunzi huyo alikutwa na ajali hiyo ya kufamaji jioni ya Julai 29, mwaka huu wakati yeye pamoja na wanafunzi wenzake watatu walipokwenda katika mto huo kufua.
Alisema wakati wanafunzi hao wakifua ghafla mwenzao huyo alivutwa na maji hayo na kupotea.
Chaula alisema ingawa taarifa ya kupotea mwanafunzi huyo ilitolewa, watu wengi walikuwa wakiogopa kuingia katika mto huo unaodaiwa kuwa na mambo ya ushirikina.
“Ndipo walipojitokeza vijana hao 15 na bila woga wakaifanya kazi hiyo hadi kesho yake saa 8.00 mchana walipoupata mwili wa mwanafunzi huyo,” alisema.
Akizungumzia mambo ya ushirikina yanayoelezwa kuwapo katika mto huo, Ackles Ngonyani ambaye ni mmoja wa vijana walioshiriki kuutafuta mwili huo, alisema; “Taarifa za miaka mingi kijijini Kiwalamo zinasema mto huo ni wa ajabu na una mambo ya ushirikina.”
Ngonyani alisema mto huo ambao maji yake ni ya baridi kama seruji, unadaiwa kuwa na nyoka wa ajabu mwenye vichwa 12 jambo linawaogopesha wananchi wengi wa kijiji hicho na maeneo jirani.
Alisema Ili kuepukana na maajabu hayo, walilazimika kupata maombi kutoka kwa wachungaji wa kijiji hicho kabla ya kuanza kuutafuta mwili wa mwanafunzi huyo.
Vijana hao walimshukuru mkuu wa wilaya kwa kutambua mchango wao katika jamii huku wakiahidi kufanya mengine mema.
Moja ya kazi itakayofanywa na Rais Magufuli kwenye ziara yake Kenya
Rais wa Tanzania John Magufuli anatarajiwa kuanza ziara yake ya kikazi katika nchi jirani ya Kenya leo.Tokeo la picha la rais maguful
Kwenye ziara hiyo ya siku mbili, Rais Magufuli anatarajiwa kufanya mazungumzo na mwenyeji wake na pia kuzindua barabara mchepuko ya Southern By-pass iliyopo Jijini Nairobi.
Barabara hiyo, ambayo inaunganisha maeneo mbalimbali ya jiji la Nairobi kwa barabara za juu na chini, ni moja kati ya miradi mbalimbali ya ujenzi wa barabara ambayo imekuwa ikitekelezwa na serikali ya Kenya kupunguza msongamano wa magari katika jiji hilo kuu.
Rais Magufuli anatarajiwa kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta Jijini Nairobi majira ya saa nne asubuhi na baadaye kupokelewa rasmi na mwenyeji wake Rais Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi ambako viongozi hao watafanya mazungumzo rasmi.
"Katika ziara hii Rais Magufuli anatarajiwa kutembelea kiwanda cha maziwa cha Eldoville kilichopo Karen Jijini Nairobi, na pia anatarajiwa kuzindua barabara mchepuko ya Southern By-pass iliyopo Jijini Nairobi," taarifa kutoka ikulu ya Tanzania imesema.
Ziara hiyo ya Rais Magufuli inajiri wakati ambao anakaribia kumaliza mwaka mmoja madarakani.
Katika kipindi hicho, hajakuwa akizuru sana mataifa ya nje na uhusiano kati ya serikali yake na serikali ya Rais Kenyatta umeonekana kuwa 'baridi kiasi'.
Tangu aingie mamlakani mwezi Novemba mwaka jana, amezuru tu Rwanda na Uganda.
Kabla ya kuchaguliwa kuwa Rais, Dkt Magufuli alikuwa amehudumu serikalini kama waziri wa ujenzi.
Taarifa kutoka ikulu ya Tanzania inasema ziara yake imetokana na mwaliko wa Rais Kenyatta.
Mavugo asema mambo ni magumu
Mshambuliaji Laudit Mavugo raia wa Burundi, bado hajafikia kile kiwango ambacho Watanzania wengi wapenda soka hasa wale wa timu ya Simba walikuwa wakikitarajia.Tokeo la picha la mavugo simba
Hali hiyo imezua maswali mengi na wakati mwingine inamuonyesha yeye kupaniki akitaka kuwaonyesha anaweza.
Lakini baadaye amekubali, kwamba anahitaji muda ili ikifika siku, ataonyesha alichonacho.
Mavugo ambaye alisajiliwa Simba akitokea Vital’O ya kwao Burundi, mara ya mwisho kufunga bao ilikuwa ni Oktoba 23 dhidi ya Toto kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar lakini kabla ya hapo alikuwa amecheza mechi sita mfululizo bila kufunga bao lolote.
Juzi Jumamosi kwenye mchezo dhidi ya Mwadui mjini hapa alishindwa tena kucheka na nyavu. Alipata nafasi kibao lakini alizipoteza kabla ya kocha Joseph Omog kumtoa katika dakika ya 42 kipindi cha kwanza.
Baada ya mchezo huo, Mavugo ambaye alianza ligi kwa mbwembwe na kuonekana atakuwa supastaa wa Simba, alisema: “Hakika naomba mashabiki wa Simba wanipe muda kwani bado sijazoea baadhi ya viwanja vya hapa Tanzania, kwani kuna viwanja vizuri lakini pia vingine ni vibovu.
“Kule kwetu Burundi hakuna viwanja vibovu kama huku Tanzania, ndiyo maana kule nilikuwa nafunga mabao mengi lakini huku napata tabu sana jinsi ya kufunga lakini nina imani kuwa nitayazoea mazingira na nitafanya vema.”
Juzi, Mavugo ambaye msimu huu tayari ana mabao manne, alikosa mabao matatu ya wazi na kulazimika kutolewa nje mapema kabisa na nafasi yake ikachukuliwa na Ame Ally aliyeiimarisha safu ya ushambuliaji ya Simba huku akitoa pasi ya bao la tatu la klabu hiyo lililofungwa na Mohammed Ibrahim.
Pamoja na papara, Mavugo amekuwa akionyesha ni mchezaji anayeweza kufanya vizuri zaidi ya alipofikia lakini papara ya kutaka kuwaonyesha wanaofikiri hawawezi wamekosea, inachangia kwa kiasi kikubwa yeye kushindwa kufanya vema kama anavyotak
Rais Magufuli kufanya ziara ya Kiserikali ya siku mbili nchini Kenya Kuanzia Kesho
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 31 Oktoba, 2016 ataanza ziara ya Kiserikali ya siku mbili nchini Kenya kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta.
Rais Magufuli anatarajiwa kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta Jijini Nairobi majira ya saa nne asubuhi na baadaye kupokelewa rasmi na mwenyeji wake Rais Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi ambako viongozi hao watafanya mazungumzo rasmi.
Pamoja na kufanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake, Rais Magufuli atakwenda kutoa heshima katika Kaburi la Rais wa Kwanza wa Kenya Hayati Mzee Jomo Kenyatta na pia anatarajiwa kuhudhuria dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa na mwenyeji wake Rais Uhuru Kenyatta Ikulu Jijini Nairobi
Katika ziara hii Rais Magufuli anatarajiwa kutembelea kiwanda cha maziwa cha Eldoville kilichopo Karen Jijini Nairobi, na pia anatarajiwa kuzindua barabara mchepuko ya Southern By-pass iliyopo Jijini Nairobi.
Barabara hiyo mchepuko ya Southern By-pass ni moja kati ya miradi mikubwa ya barabara nchini Kenya, inaunganisha maeneo mbalimbali ya Jiji la Nairobi kwa barabara za juu na chini na imejengwa kwa lengo la kupunguza msongamano wa magari katika Jiji hilo.
Rais Magufuli anatarajiwa kumaliza ziara yake tarehe 01 Novemba, 2016 na kurejea Jijini Dar es Salaam.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Breaking news:BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU TANZANIA IMETANGAZA RASMI KWA WANAFUNZI WOTE WALIOOMBA MKOPO KUANGALIA SASA MIKOPO WALIYOPANGIWA 2016/2017
Image result for OLAS.GO.TZ
Bodi ya mikopo ya elimu ya juu Inawatangazia waombaji wote wa mwaka wa masomo 2016/2017 ,kuangalia mikopo waliyopangiwa.
Kama utahitaji kuangaliziwa jina lako kwa "usahihi" na "kasi ya ajabu" (ambapo utajibiwa ndani ya dk 1 tu) kama limepata mkopo tafadhali fanya yafuatayo;
1.TUMA EXAM NAMBA YAKO YA FORM 4 NA MWAKA
ULIOMALIZA MFANO:S3409.0012.2013-HESLB KWENDA
NAMBA 0717647448
2.HUDUMA HII UTATOZWA TSHS 1000 TU(KWA AJILI YA
KUISUPORT MASWAYETU BLOG)
3.TUMA PESA KWENDA 0717647448-MPESA
0717647448 -TIGO PESA
&AIRTELY MONEY
4.UTAJIBIWA NDANI YA DK 1 TU.
5.TUMA PESA KWANZA,NDIO UTAJIBIWA SMS YAKO
Kindly Click here to view your Loan allocation status. Please note that you will be required to use the four index number you used during your application.
BREAKING NEWS: BONDIA MASHALI AFARIKI DUNIA - AUWAWA, MWILI WAKE WAOKOTWA VICHAKANI DAR
Bondia maarufu wa ngumi za kulipwa nchini, Thomas Mashali, hatunaye.
Taarifa zinaeleza ameuwawa kwa kupigwa risasi na mwili wake kuokotwa vichakani maeneo ya Kimara jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia leo.
Yassin Abdallah maarufu kama Ustaadhi, mmoja wa viongozi wakongwe wa mchezo wa ngumi amethibitisha na kusema mwili wa Mashali upo kwenye chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.
"Tumethibitishiwa hizo taarifa za majonzi kabisa, mwili upo Muhimbili na msiba upo kwao Tandale," alisema Ustaadhi.
Friday, October 28, 2016
Burudani Alikiba aelezea ujio wa single mpya aliyoshirikishwa na Ommy Dimpoz
Ni October 28, 2016 ambapo mkali kutoka Bongo Flevani, Alikiba amefunguka na kuweka wazi ujio wa single mpya aliyoshirikishwa na Ommy Dimpoz iitwayo Kajiandae.
Staa huyo akizungumza kwenye kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa kupitia Clouds TV aliyaongea haya>>>>Kiukweli kwanza ni wimbo mzuri pili maandalizi ya video hiyo tayari tumeshafanya na jina la wimbo unaitwa Kajiandae kwahiyo mashabiki wangu na mashabiki wa Ommy Dimpoz wakati wowote watapata ladha nzuri tu kwani najua ni kitu gani mashabiki wa muziki wangu wanachokitaka kutoka kwangu’
Michezo BREAKING NEWS: Usishangae kumuona kocha Hans van Pluijm akiifundisha Yanga tena
Siku nne baada ya aliyekuwa kocha mkuu wa klabu ya Dar es Salaam Young Africans muholanzi Hans van Pluijm ajiuzulu nafasi yake hiyo, leo October 28 2016 klabu ya Yanga imemuandikia barua ya kumuomba abadili maamuzi yake ya kujiuzulu na arejee kazini kama kawaida.
Baada ya uongozi wa klabu ya Yanga kupitia kwa kaimu katibu mkuu wake Baraka Deusdedit pamoja na waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mwigulu Nchemba ambaye pia ni shabiki wa Yanga na mwanachama, wamemuomba kocha Hans van Pluijm atengue uamuzi wake wa kujiuzulu na kurudi kazini kama kawaida.
Kwa maamuzi hayo ya Yanga kumuomba kocha Hans van Pluijm arudi usishangae ukimuona akirejea katika benchi la Yanga kwa siku za karibuni, inaripotiwa kuwa maamuzi ya Yanga kuandika barua hiyo yaliafikiwa baada ya kukaa na kufanya maongezi na kocha Hans van Pluijm kwa siku tatu pamoja na katibu na waziri Mwigulu.
BREAKING NEWS: Usishangae kumuona kocha Hans van Pluijm akiifundisha Yanga tena
Siku nne baada ya aliyekuwa kocha mkuu wa klabu ya Dar es Salaam Young Africans muholanzi Hans van Pluijm ajiuzulu nafasi yake hiyo, leo October 28 2016 klabu ya Yanga imemuandikia barua ya kumuomba abadili maamuzi yake ya kujiuzulu na arejee kazini kama kawaida.
Baada ya uongozi wa klabu ya Yanga kupitia kwa kaimu katibu mkuu wake Baraka Deusdedit pamoja na waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mwigulu Nchemba ambaye pia ni shabiki wa Yanga na mwanachama, wamemuomba kocha Hans van Pluijm atengue uamuzi wake wa kujiuzulu na kurudi kazini kama kawaida.
Kwa maamuzi hayo ya Yanga kumuomba kocha Hans van Pluijm arudi usishangae ukimuona akirejea katika benchi la Yanga kwa siku za karibuni, inaripotiwa kuwa maamuzi ya Yanga kuandika barua hiyo yaliafikiwa baada ya kukaa na kufanya maongezi na kocha Hans van Pluijm kwa siku tatu pamoja na katibu na waziri Mwigulu.
Mix Ubalozi wa Marekani nchini Kenya wafungwa baada ya tukio la kisu
Jana October 27 2016 iliripotiwa taarifa ya mwanaume mmoja kujaribu mshambulia afisa wa usalama karibu na ubalozi wa Marekani nchini Kenya kwa kisu, kisa hicho kimefanya ubalozi wa Marekani nchini Kenya leo October 28 2016 kutangaza kufungwa kwa muda kwa ubalozi huo.
Mwanamume aliyejaribu kumshambulia afisa wa usalama kwa kupigwa risasi, Imeeelezwa hakuna afisa yeyote wa ubalozi huo aliyeathiriwa na kisa hicho.
Leo October 28 2016 Taarifa zilizotolewa kwenye tovuti ya ubalozi imesema ……..>>>Ubalozi utafungwa October 28 2016 na huduma zote za kibalozi zimesitishwa, lakini huduma za kibalozi za dharura kwa raia wa Marekani zitaendelea kutolewa’
Basi la Hood lagongana na lori na kupinduka kwenye mlima Kitonga
Basi la kampuni ya Hood linalofanya safari zake kati ya Mbeya na Arusha jana mchana lilipata ajali na kupinduka katika mlima Kitonga mkoani Iringa baada ya kugongana na lori la mafuta.
Katika ajali hiyo mtu mmoja amepoteza maisha na wengine 43 wamejeruhiwa. Kati ya majeruhi hao 25 wapo Hospitali ya Itunda Ilula na 18 wapo katika Hospitali ya Mkoa.
UDOM:TAARIFA MAALUM KWA WANAFUNZI WA UDOM
PAYMENT OF TUITION FEES AND DIRECT COSTS:
ALL STUDENTS ARE REQUIRED TO PAY TUITION FEES AND DIRECT COSTS FOR THE ACADEMIC YEAR 2016/2017 BY 28TH OCTOBER 2016. STUDENTS WHO WILL FAIL TO COMPLY WITH THIS NOTICE WILL NOT BE ALLOWED TO CONTINUE WITH THEIR STUDIES.PAYMENT MUST BE MADE BEFORE STUDENTS REPORT TO THE UNIVERSITY.
CONTINUING STUDENTS WITH OUTSTANDING BALANCE ARE REQUIRED TO PAY THEIR DUES APART FROM THE
2016/2017 FEE. STUDENTS SHOULD COME WITH THEIR BANK DEPOSIT SLIPS ON REPORTING.
FURTHER, ALL STUDENTS ARE REQUIRED TO PROVIDE THE FOLLOWING INFORMATION TO THE BANKERS ON MAKING PAYMENTS:
NAME OF STUDENT : JACKLINE, PROSPER M
REGISTRATION NUMBER : EG T/UDOM/2012/000432
DEGREE PROGRAMME : BCOM FINANCE
YEAR OF STUDY : EG 1 OR 2 OR 3 OR 4
STUDENT ORGANIZATION FEE AND HEALTH INSURANCE SHOULD BE PAID TO THE RESPECTIVE ORGANIZATIONS
ALL PAYMENTS SHOULD BE DONE AT THE BANK BRANCHES AND NOT TO THEIR AGENTS.
Important-notice-to-all-students-2016-2017 NHIF – TANGAZO LA WANAFUNZI
Mafanikio Ya Kiuchumi Kutokana Na Jitihada Mbali Mbali Zilizofanywa Na Serikali Ya Awamu Ya Tano Katika Kipindi Cha Mwaka Mmoja - Benki Kuu Ya Tanzania
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli,
alipoingia madarakani mwezi Novemba 2015 aliendeleza jitihada za kukuza uchumi wa nchi yetu kwa kuweka mkazo na kutoa maagizo kwenye maeneo kadhaa yakiwemo; kuongeza nguvu kwenye ukusanyaji wa kodi, kupiga vita rushwa, kuweka msisitizo mkubwa wa nidhamu ya matumizi ya fedha za umma, kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na kuelekeza matumizi katika sekta za vipaumbele vya maendeleo. Aidha, kuzitaka Wizara, Wakala na Taasisi za Umma kuweka fedha zao Benki Kuu na kuhimiza kila mtu afanye kazi na kula kwa jasho lake ili kutekeleza falsafa ya ‘Hapa kazi tu’.
Maagizo haya yamekuwa kichocheo cha ukuaji mzuri wa uchumi. Kupitia maagizo haya Benki Kuu tunaweza kuelezea mafanikio kadhaa yaliyopatikana katika kipindi hiki kama ifuatavyo;
1. Kuimarisha ukusanyaji wa mapato, kuziba mianya ya ukwepaji kodi na kuelekeza matumizi katika sekta za vipaumbele vya maendeleo
· Tangu Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakani mnamo Novemba mwaka 2015, makusanyo ya mapato yameendelea kuongezeka. Kwa mfano, kati ya Januari hadi Septemba 2016, makusanyo ya mapato ya ndani yalikuwa shilingi bilioni 11,174 ikiwa ni wastani wa shilingi bilioni 1,241.55 kwa mwezi, ikilinganishwa na wastani wa shilingi bilioni 950.22 katika kipindi kama hicho kwa mwaka 2015. Makusanyo ya mapato ya ndani katika 2016 yalitosheleza matumizi yote ya kawaida (recurrent) na kubakiza ziada kwa ajili ya ulipaji wa madeni ya nje (amortization) na sehemu kubwa ya matumizi kwa ajili ya shughuli za maendeleo.
Ukuaji wa Pato la Taifa (Real GDP)
· Uchumi umeendelea kukua kwa kiwango kikubwa kutokana na sera nzuri za uchumi mpana (macroeconomic policies). Kasi ya ukuaji wa pato la Taifa katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016, yaani Januari-Juni 2016, imeongezeka na kufikia asilimia 6.7 ikilinganishwa na asilimia 5.7 kwa nusu ya kwanza ya mwaka 2015. Ukuaji huu umechangiwa na kukamilika kwa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam na kuanza kutumia gesi katika kuzalisha umeme, usafirishaji, ukiwemo usafiri wa abiria kutumia reli na mabasi ya mwendo kasi (UDART); kuongezeka kwa matumizi ya simu za mkononi, uzalishaji wa gesi, vyuma na bidhaa zisizo za vyuma pamoja na kuimarika na kupanuka kwa huduma za kifedha. Sekta za uchumi zilizoongoza katika kasi ya ukuaji ni usafirishaji (asilimia 17.4), madini (mining and quarrying) (13.7), fedha na bima (asilimia 8.7), uzalishaji viwandani (manufacturing) (asilimia 8.3) na elimu (asilimia 8.0) kutokana na sera ya utoaji wa elimu ya msingi bila malipo iliyoanza Januari 2016.
Mfumuko wa bei
· Mfumuko wa bei ulibakia katika kiwango cha tarakimu moja (single digit) kutokana na sera nzuri ya fedha na ile ya bajeti pamoja na kupungua kwa bei za bidhaa duniani kote. Katika mwaka ulioishia Septemba 2016, mfumuko wa bei ulikua kwa asilimia 4.5 ikilinganishwa na asilimia 6.1 kaitka kipindi kama hicho mwaka 2015 na lengo la muda wa kati la asilimia 5.0. Kutokana na sera za uchumi mpana, pamoja na kuimarika kwa shilingi dhidi ya dola ya Marekani na bei ndogo za mafuta katika soko la dunia, mfumuko wa bei unatarajiwa kubakia karibu na lengo la kiwango cha muda wa kati cha asilimia 5.0.
Shughuli za Serikali
· Serikali ya awamu ya tano ilianza katika kipindi ambacho upatikanaji wa misaada ya kibajeti (GBS) ulikuwa siyo mzuri kutokana na kubadilika kwa sera za maendeleo za kimataifa (foreign development policies) katIka nchi wahisani ambapo mwelekeo ulikuwa ni kupeleka fedha za miradi moja kwa moja. Pamoja na nchi nyingi wahisani kujitoa katika kusaidia katika bajeti (GBS), Serikali ya awamu ya tano imeweza kushirikiana na wadau wa maendeleo (DPs) katika kutafuta njia mbadala za kuziba pengo hilo.
2. Uimarishaji Wa Ukusanyaji Wa Mapato Uliendana Na Uimarishaji Wa Mazingira Mazuri ya Kibiashara
· Sera nzuri za uchumi (macroeconomic policies) za awamu ya tano zimeendelea kukwamua na kuimarisha mazingira ya biashara. Hii imejidhihirisha katika kuimarika kwa nakisi katika urari wa biashara (current account deficit) katika miezi tisa ya mwazo ya 2016. Nakisi ya urari wa biashara imepungua sana, kufikia dola za Marekani millioni 1,621.8 katika mwezi tisa ya 2016 kutoka nakisi ya dola milioni 3,715.5 katika kipindi kama hicho mwaka 2015. Hii ni kutokana na kuongezeka kwa mauzo ya nje ya bidhaa na huduma (utalii, dhahabu, bidhaa za viwandani), pamoja na kupungua kwa kiwango kikuwa kwa uagizaji wa bidhaa na huduma (mitaji, mafuta, chakula na bidhaa za chakula).
Thamani ya Shilingi
· Kutokana na sera nzuri za Serikali ya Awamu ya Tano, thamani ya shilingi imebaki kuwa imara (wastani wa shilingi 2,178.6 kwa dola ya Marekani) ikilinganishwa na dola ya Kimarekani na sarafu zingine za nchi jirani na nchi washirika wa kibiashara. Kutokuyumba kwa shilingi kumechangiwa na kuimarika kwa uchumi; kuhamishwa kwa fedha za mashirika ya umma kutoka mabenki ya biashara kwenda Benki Kuu; kupunguzwa kwa matumizi yasiyo ya lazima ya Serikali na kutoterereka kwa Akiba ya Fedha za Kigeni.
Akiba ya Fedha za Kigeni
· Akiba ya fedha za kigeni imebaki kuwa imara, ikiwa ni dola za Marekani milioni 4,096.0 kufikia mwisho wa mwezi Septemba 2016, ambao ni uwezo wa kutosheleza uagizaji nje wa bidhaa na hudumu kwa kipindi cha miezi 4. Kuongezeka (kutotetereka) kwa Akiba ya Fedha za Kigeni kunatokana na manunuzi yanayofanywa na Benki Kuu kutoka kwenye soko la ndani la fedha za kigeni na mashirika ya umma.
3. Kuhamisha Fedha za Mashirika ya Umma kutoka katika Mabenki Binafsi kwenda Benki Kuu ya Tanzania
Serikali ya Awamu ya Tano iliagiza utekelezaji wa Sheria ya Benki Kuu ya mwaka 2006, hasa Sura ya 32 inayohusu utunzaji wa amana za mashirika ya umma na taasisi za serikali. Imechukua miaka tisa kuanza kutekeleza masharti ya hiyo kuhusu akaunti za Mashirika ya Umma, Idara za Serikali na Serikali za Mitaa. Kuchelewa huku, kulizifanya benki nyingi za biashara zitumie fedha hizo za umma kununua Dhamana za Serikali na Hati Fungani na hivyo kuifanya Serikali kuuziwa fedha zake yenyewe. Biashara hiyo sasa imekoma kutokana na hatua madhubuti za kuitekeleza sheria hiyo.
Hatua hizo zimewezesha kupatikana na kwa mafanikio yafuatayo:
(a) Kufungua akaunti za amana za Mashirika ya Umma na Idara za Serikali: Kati ya Novemba 2015 hadi Oktoba 26, 2016, jumla ya akaunti 267 zenye jumla ya amana za Shilingi 206,913,915,522.06 zimefunguliwa. Aidha, baadhi ya taasisi hizo zimefungua akaunti za fedha za kigeni 131 zenye Dola 163,480,125.75, sawa na shilingi 357,694,000,000.00. Hivyo jumla ya amana zote za shilingi na fedha za kigeni za mashirika na taasisi za umma zinazotunzwa Benki Kuu ni shilingi 564,608,460,663.00
(b) Amana za akaunti za Serikali za Mitaa: Serikali imeamua kufungua akaunti maalum kwa ajili ya kutunza amana za Serikali za Mitaa. Mradi huu umeanza kutekelezwa kuanzia mwezi Aprili 2016 na mpaka sasa jumla ya mikoa mitano imeunganishwa. Mikoa hiyo ni Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Mbeya na Mwanza. Mpaka tarehe 26 Oktoba 2016, amana za halmashauri za mikoa hiyo mitano ambazo zipo Benki Kuu ya Tanzania zinafikia kiasi cha shilingi 108,387,942,351.15. Bila kukamilisha sehemu ya mradi huu, fedha hizi zingekuwa kwenye benki za biashara.
Matokeo:
· Kwa upande Serikali;
·Kumeleta uwazi kuhusu mapato na matumizi ya mashirika hayo
·Kupungua kwa gharama za usimamizi wa ujazi wa fedha (liquidity management) kwenye mzunguko.
· Kwa mabenki;
·kumeleta usawa katika ushindani kati ya mabenki badala ya wachache kunufaika kwa kupata amana za mashirika ya umma.
·kumeleta ubunifu kwa mabenki katika kubuni bidhaa (bank products) mbali mbali mpya ili kujiongezea amana.
·Kutokana na Sera ya Fedha ambayo ni rafiki, malengo mapana ya Serikali, ukuaji wa uchumi na ukuaji wa fedha ukuwa ndani ya malengo.
·Katika kipindi cha miezi tisa ya 2016, amana katika mabenki ya biashara zimeongeza kutoka asilimi 9.84 katika miezi tisa ya mwanzo wa mwaka 2015 na kufikia asilimia 11.59 kaitka miezi tisa yam waka 2016. Vile vile, riba za mikopo kwa mwaka mmoja zilipungua kutoka wastani wa asilimia 15.49 na kufikia asilimia 13.87
·Mwenendo huu wa riba ulipelekea kupungua kwa tofauti kati ya riba za mkopo na zile za amana kutoka wastani wa asilimia 5.92 ilivyokuwa katika miezi tisa ya mwanzo ya 2015 na kufikia wastani wa asilimia 2.28 katika miezi tisa ya 2016, ikimaanisha kupugua kwa gharama za mikopo.
Mafanikio mengine
4. Mwenendo wa Sekta ya Kibenki
Katika kipindi cha kuanzia Septemba 2015 hadi September 2016, sekta ya kibenki imeendelea kukua ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa taasisi mpya za kifedha ikiwemo Benki ya Waalimu Tanzania (Mwalimu Commercial Bank Plc) na Canara Bank (Tanzania) Limited. Takwimu zinaonesha kuwa mabenki yetu ni imara na salama, yakiwa na mitaji na ukwasi wa kutosha. Kufikia mwezi Septemba 2016, kulikuwa na jumla ya benki na taasisi za fedha zinazosimamiwa na Benki Kuu zipatazo 66 zenye matawi 750 nchini kote, ikilinganishwa na taasisi 62 zilizokuwa na matawi 715 mwezi Septemba 2015.
Katika kipindi hicho, benki mbili - Guaranty Trust Bank Tanzania Ltd na Yetu Microfinance Bank Plc na taasisi ya fedha moja ya M Mortgages Tanzania Ltd zilipata leseni za muda.
Kiwango cha mitaji kikilinganishwa na mali iliyowekezwa (total capital to total risk weighted assets and off-balance sheet exposures) kilikuwa asilimia 19.24 kikilinganishwa na kiwango cha chini kinachotakiwa kisheria cha asilimia 12. Hali ya ukwasi, ambayo hupimwa kwa kuangalia uwiano kati ya mali inayoweza kubadilishwa kuwa fedha taslimu na amana zinazoweza kuhitajika katika muda mfupi (liquid assets to demand liabilities), ulikuwa asilimia 34.18 ukilinganishwa na uwiano wa chini unaohitajika kisheria wa asilimia 20.
Mpaka kufikia Septemba 2016, mikopo chechefu ilikuwa wastani wa asilimia 9.06 ikilinganisha na wastani wa asilimia 6.61 ya Septemba 2015. Mikopo chechefu imeendelea kuwa ni changamoto katika sekta ya kibenki kutokana na ufanisi mdogo wa urejeshaji mikopo katika sekta ya kilimo na biashara.
Amana za wateja katika mabenki zilipungua kutoka shilingi trilioni 20.19 mwezi Oktoba 2015 hadi kufikia shilingi trilioni 20.01 mwezi Septemba 2016. Miongoni mwa sababu zilizochangia kupungua kwa amana kwenye mabenki ni pamoja na uamuzi wa Serikali kuhamisha sehemu ya fedha za taasisi na mashirika ya umma kutoka mabenki ya biashara kwenda Benki Kuu ya Tanzania. Aidha, mikopo (loans and overdafts) iliongezeka kutoka shilingi za Kitanzania trilioni 14.48 mwezi Oktoba 2015 hadi kufikia shilingi trilioni 15.74 mwezi Septemba 2016.
Jumla ya rasilimali (Total assets) za mabenki na taasisi za fedha ziliongezeka kwa asilimia 4.71 kutoka shilingi trilioni 26.57 mnamo Septemba 2015 mpaka shilingi trilioni 27.82 mwisho wa Septemba 2016. Kwa kipindi cha miezi tisa kufikia Septemba 2016, jumla ya faida baada ya kodi katika sekta ya kibenki iliongezeka kufikia shilingi trilioni 352.37 ikilinganishwa na shilingi trilioni 344.87 katika kipindi kilichoishia Septemba 2015.
Upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wananchi umeendelea kuongezeka kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya teknolojia katika utoaji wa huduma za malipo ya rejareja kupitia simu za mkononi, pamoja na huduma za kibenki kupitia mawakala (agent banking services).
Mabenki yameendelea kutumika katika kutunza fedha na mitaji ya wateja na kurahisisha miamala au malipo kwa wateja wake. Ili kulinda maslahi ya wateja na amana zao, Benki Kuu ya Tanzania imeendelea kutunga sheria, kanuni na miongozo inayotumiwa na mabenki na kusimamia utekelezaji wake.
Katika kipindi husika, Benki Kuu ya Tanzania imeendelea na jukumu lake la kusimamia na kudhibiti mabenki na taasisi za fedha kwa niaba ya Serikali ya Tanzania. Benki Kuu, imeendelea kuhakikisha kuwa mabenki na taasisi za fedha zina mikakati inayokidhi vigezo muhimu (minimum standards) kwa kupitia ukaguzi wa mabenki unaofanyika mara kwa mara.
Maduka ya Kuuza Fedha za Kigeni
Idadi ya Maduka ya Kuuza Fedha za Kigeni (bureaux de change) imefikia 290 ikilinganishwa na maduka 266 yaliyokuwepo Septemba 2015. Mpaka kufikia Septemba 2016, maduka yapatayo 260 yalikuwa yanafanya biashara Tanzania Bara na 30 Tanzania Visiwani, ikilinganishwa na maduka 239 Tanzania Bara na 27 Tanzania Visiwani yaliyokuwa yanafanya biashara kufikia Septemba 2015.
Benki Kuu inasimamia usalama, utulivu na uthabiti wa sekta ya benki Tanzania. Inalinda wateja wanaoweka amana zao kwenye mabenki na taasisi za fedha. Mabenki yanaendelea kutoa mchango mkubwa kwenye kukuza uchumi wa nchi; kuongeza ushindani kwenye sekta ya kibenki na kuzuia matumizi mabaya ya sekta ya kifedha. Benki Kuu imeendelea kupima ustahimilivu wa mabenki wakati inapojitokeza hali ambayo inaweza kuathiri mapato na mitaji ya mabenki hayo (Stess testing). Pia, husaidia katika kutoa mwelekeo wa Sera ya kifedha nchini.
Sekta ya kibenki imeendelea kushuhudia mabadiliko makubwa katika aina za huduma zitolewazo na katika njia zinazotumika kutoa huduma hizo. Mabadiliko hayo ni pamoja na; Huduma za kibenki kwa kufuata misingi ya Shariah; Huduma za kibenki kupitia wakala; Huduma za kifedha kupitia simu za mikononi na
Benki Kuu imeendelea kusimamia benki mbili za maendeleo (TIB na TADB) ili ziweze kutoa mikopo katika sekta mbalimbali na kuweza kuharakisha maendeleo hapa Tanzania.
Mfumo wa Upashanaji wa Taarifa za Wakopaji
Mfumo wa upashanaji taarifa za wakopaji umeendelea kuleta mafanikio makubwa katika kuboresha upatikanaji wa mikopo kutoka kwenye mabenki na taasisi za fedha zinazosimamiwa na Benki Kuu, pamoja na taasisi nyingine zinazotoa mikopo(SACCOS, MFIs, Utility Companies, Car Dealers na HESLB).
Mfumo huo unajumuisha utaratibu wa kuweka taarifa za wakopaji kupitia Benki Kuu (Credit reference databank), na makampuni binafsi yaliyoruhusiwa kubadilishana taarifa za wakopaji na mabenki na taasisi nyingine zinazotoa mikopo. Kufikia Septemba 2016 jumla ya wakopaji waliokuwa katika mfumo huo walikuwa zaidi ya 1,600,000 ikilinganishwa na zaidi ya 900,000 ya Septemba 2015.
Jumla ya mikopo mpaka kufikia Septemba 2016 ilikuwa ni zaidi ya 3,000,000 ukilinganisha na zaidi ya 1,690,000 ya Septemba 2015. Katika taarifa ya mazingira ya biashara (World Bank Doing Business Report, 2017), Tanzania imefanya vizuri kutoka nafasi ya 152 hadi 44 kati ya nchi 190 zilizofanyiwa utafiti huo.
Mifumo ya Malipo Nchini
Benki Kuu imeendelea na kazi yake ya kisheria ya kusimamia mifumo ya malipo nchini ambapo Sheria ya Mifumo ya Malipo Nchini 2015 imeanza kufanya kazi. Chini ya sheria hii zimeanzishwa kanuni mbili za uendeshaji wa mifumo. Kanuni hizo ni pamoja na Kanuni ya Leseni na Vibali kwa Watoa Huduma za Mifumo ya Malipo 2015 pamoja na Kanuni za Kutoa Fedha za Kielektroniki 2015. Uwepo wa Sheria umeimarisha usalama katika mifumo ya malipo nchini na kuongeza ufanisi katika usimamizi wa mifumo ya malipo ya taifa.
Kwa kipindi hiki, huduma za fedha jumuishi (financial inclusion) imeongezeka kwa kiasi kikubwa ikichangiwa na usalama uliopo kwenye mifumo ya malipo. Aidha, idadi ya watumiaji wa huduma za fedha kwa njia ya mtandao imeendelea kuongezeka kwa kasi kubwa.
Kutokana na maendeleo haya, wananchi wamefaidika kwa kupata huduma mbali mbali za kifedha kama vile, kutuma na kupokea, kutunza fedha, huduma za bima, huduma za mikopo midogo midogo. Kadhalika, huduma za malipo ya ada mbali mbali kama vile ada za shule, kodi ndogo ndogo, faini ya makosa ya barabarani na malipo ya huduma kama za maji, umeme na televisheni. Benki kuu inaendelea kushirikiana na wadau wengine wa serikali ili kuahakikisha kuwa mifumo hii ya malipo pia inatumiwa katika kukusanya mapato ya serikali.
Aidha, kuanzia Februari 2016, Tanzania imekuwa nchi ya kwanza duniani kuweza kufanikisha malipo ya moja kwa moja kutoka mtandao mmoja kwenda mwingine (wallet to wallet interoperability). Mafanikio haya yatawezesha wananchi kupata huduma za kifedha kwa mtandao kwa urahisi na unafuu zaidi.
Uboreshwaji wa huduma za malipo ya serikali kwa njia ya kieletroniki kama mbadala wa malipo kwa njia ya cheki za serikali, baada ya kuanzisha mfumo maalumu wa malipo ya serikali ambayo unasaidia sasa serikali kulipa mishahara, pensheni pamoja na mirathi bila kutumia cheki. Mfumo huu umesaidia kuleta uharaka na usalama katika malipo ya serikali na kupunguza mianya ya wizi uliokuwa unafanywa na wahalifu kutokana na mapungufu ya mfumo wa utoaji wa cheki za serikali. Aidha ili kusaidia malipo ya mishahara, Benki kuu pia iliongeza kiwango cha ukomo wa malipo kwa njia ya kutumiana kwenye akaunti za kibenki (Electronic Fund Transfer (EFT)) kutoka Milioni Kumi (10,000,000) ya awali hadi Milioni Ishirini (20,000,000/=) ili kuiwezesha serikali kulipa malipo mengi zaidi kwa njia hii.
Ili kuongeza matumizi ya malipo kwa njia ya kieletroniki katika halimashauri, Benki kuu iliamua kuunganisha halmashauri kwenye mfumo wa Malipo wa TISS (Tanzania Interbank Settlement System (TISS). Hadi sasa halmashauri zote katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza (isipokuwa Ilemela and Buchosa), Arusha, Mbeya (isipokuwa Busekelo), Dodoma (isipokuwa Kondoa and Chemba) na Songwe (isipokuwa Songwe and Tunduma) zimekwishaunganishwa, pamoja na hazina ndogo zote 24. Hali hii imesaidia kuongeza udhibiti wa malipo ya serikali pamoja na ufanisi katika ulipaji, hali ambayo imesaidia serikili kwa kiwango kikubwa kutekeleza malengo yake.
Katika juhudi za serikali kurahisisha na kuleta ufanisi katika ukusanyaji wa kodi na maduhuli mbali mbali, Benki Kuu imeendelea kufanikisha unganishwaji wa watoa huduma mbali mbali katika mifumo yake ya malipo. Kwenye mfumo wa TACH, Benki kuu imefanikiwa kuongeza Benki nne (4) tangu katika kipindi kifupi ambazo ni TIB Corporate Bank (December 2015), Tanzania Postal Bank (April 2016), Canara Bank Tanzania Ltd (September 2016) na Mwalimu Commercial Bank Plc (October 2016). Aidha, kwenye mfumo wa TISS, Benki Tatu (3) zaidi zimejiunga ambazo ni Canara Bank Tanzania Ltd , Meru Community Bank na Mwalimu Commercial Bank Plc. Kujiunga kwa Benki hizi kwenye mifumo ya malipo ya Benki kuu, imeongeza wigo wa watoa huduma walio tayari kukusanya mapato ya serikali sehemu mbali mbali.
Ili kuunga mkono juhudi za serikali za kukusanya kodi na mapato mengine, Benki kuu imeongeza muda wa kuendesha mifumo yake ili kuwangezea walipaji muda zaidi wa kufanya malipo kupitia mifumo hii. Muda wa mfumo wa TISS kufanya kazi umeongezwa kutoka saa 10 jioni hadi saa 2 za usiku. Aidha sasa hivi mfumo huu unafunguliwa pia siku za jumamosi na jumapili kinyume na hapo awali.
Benki kuu imeendelea kushirikiana na nchi nyingine za jumuiya ya Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla ili kutengeneza na kuendeleza mifumo ya malipo inayovuka mipaka. Mfumo wa malipo wa Afrika Mashariki (East African Cross Border Payment System) umeendelea kuboreshwa ili uweze kutumiwa zaidi na wananchi wanaofanya malipo ndani ya nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki. Katika kipindi hiki, malipo yanayopita kwenye mfumo huu yamezidi kuongezeka, hususa ni yale yanayofanywa kati ya Tanzania na Kenya.
Mifuko ya Udhamini wa Mikopo
Benki Kuu, ambayo ni wakala wa Serikali kupitia Kurugenzi ya Masoko ya Fedha, husimamia Mifuko ya Udhamini wa Mikopo itolewayo na mabenki kwa sekta binafsi pamoja na sekta zinazojihusisha na uzalishaji na uuzaji wa mazao nje ya nchi. Kwa sasa Benki Kuu inasimamia mifuko miwili ambayo ni Mfuko wa Udhamini wa Mauzo Nje ya Nchi (ECGS) na Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa Wajasiriamali Wadogo na wa kati (SME-CGS).
Katika kipindi cha Novemba 2015 mpaka Oktoba 2016 dhamana zenye thamani ya:
- Shilingi 130,867,038,874.85 zilitolewa chini ya Mfuko wa Udhamini wa Mauzo Nje ya Nchi (ECGS). Kupitia mfuko huu, mabenki yameweza kukopesha vyama vikuu vya Ushirika na vya Msingi vinavyojishughulisha na ununuzi wa mazao na pembejeo za kilimo. Hali kadhalika; na
- Shilingi 918,318,215 zilitolewa chini ya Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa Wajasiriamali Wadogo na wa kati (SME-CGS). Mikopo hiyo ilitolewa kwenye sekta za kilimo na ujenzi.
Huduma za Kibenki
Uharaka wa malipo ya mishahara ya wafanyakazi wa serikali: Kwa karibu kipindi cha miezi 11 sasa tangu Novemba 2015, mishahara imekuwa ikilipwa kwa wakati na mara nyingi imekuwa ikilipwa kabla ya tarehe 25 ya mwezi husika ikilinganishwa na siku za nyuma.
Kuchelewa kulipa mishahara kumekuwa kukitokana na uhaba wa fedha hasa baada ya ukomo wa kukopa kufikia mwisho. Hii haikuwa mwenendo mzuri kwani wafanyakazi hawakuwa na uhakika wa siku ya kulipwa mshahara.
Kuongezeka kwa matawi ya Benki Kuu: Moja ya majukumu ya Benki Kuu ya Tanzania ni kusambaza fedha katika matawi yake. Hadi June 2016, Benki Kuu ilikuwa na matawi matano, nayo ni; Mwanza, Arusha, Mbeya, Zanzibar na Dodoma.
Kwa vile Tanzania ina eneo kubwa; shughuli hii imekuwa na changamoto za usambazaji wa noti na sarafu katika maeneo ambayo Benki Kuu haina matawi yake. Ili kukabiliana na changamoto hii Benki Kuu imesaini mikataba na mabenki ya biashara ya usambazaji wa noti na sarafu kama ifuatavyo: -
(i) Benki ya CRDB katika mikoa ya Mtwara, Kigoma, Sumbawanga, Songea na Tanga
(ii) NMB katika mkoa wa Tabora
(iii) NBC katika mikoa ya Shinyanga na Bukoba
(iv) PBZ katika kisiwa cha Pemba
Vituo hivi vyote vimekuwa vikifanya kazi kwa ufanisi; lakini kumekuwa na changamoto mbalimbali; kubwa ikiwa ni udogo wa maghala yake kuhifadhi mahitaji halisi ya noti na sarafu kwa muda muafaka. Hali hii huilazimisha Benki Kuu kupeleka pesa mara kwa mara na hivyo kuongeza gharama za uendeshaji.
Kutokana na changamoto hizi, Benki Kuu imejenga tawi jipya katika mkoa wa Mtwara ambalo limeanza kazi rasmi mefunguliwa tarehe 3 Octoba 2016. Benki Kuu inaamini kuwa tawi hili jipya litakuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi kwenye eneo la kusini mwa Tanzania.
Miradi mikubwa ya viwanda na miundombinu inayoendelea na inayotarijiwa kuanza kazi siku za usoni itachangia katika kuimarisha uchumi.
Ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard gauge)
Ujenzi wa bomba la mafuta la Uganda ambalo litahusu vile vile upanuzi wa bandari ya Tanga
Ujenzi wa Export Processing Zone ya Kurasini – itakayokuwa mhimili wa biashara kati ya China na Ukanda huu wa Afrika
Mradi wa kuzalisha megawati 240 za umeme wa Kinyerezi II unaoendelea kujengwa.
Miradi ya kupanua viwanja vya ndege nchini kwa mfano- Dodoma, na mingine inayoendelea -katika viwanja vya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya n.k.
Ujenzi wa maghala ya taifa ya kuhifadhi chakula yenye uwezo wa kuhifadhi tani 350 yatakayojengwa kwa msaada wa Serikali ya Hungary katika sehemu mbalimbali nchini hususan katika mikoa inayozalisha mazao ya nafaka kwa wingi.
Kiwanda cha kuzalisha saruji cha Dangote kilichopo Mtwara ambacho kipo mbioni kuzalisha kulingana na uwezo wake (full capacity);
Kiwanda cha kutengeneza marumaru cha Mkuranga, Pwani ambacho ujenzi wake unaendelea
Kiwanda cha kuzalisha mbolea mkoani Lindi - kinajengwa
Kiwanda cha bidhaa za chuma – mkoani Pwani ambacho kiko mbioni kukamilika.
Hitimisho
Maagizo mbali mbali yaliyotolewa na Serikali ya Awamu ya Tano yamechochea ukuaji wa uchumi katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Mwenendo wa viashiria mbalimbali vya shughuli za uchumi unadhihirisha kwamba hali ya uchumi wa Tanzania ni nzuri na inatoa matumaini makubwa. Matarajio ni kwamba endapo shughuli halali za kiuchumi zitaendelea kutekelezwa, lengo la ukuaji wa pato la Taifa la asilimia 7.2 kwa mwaka 2016 litafanikiwa. Hii inachangiwa pia na ukweli kwamba serikali ya awamu ya tano imejipanga katika kuimarisha uchumi endelevu usiokuwa na mianya ya rushwa; usimamizi thabiti wa rasilimali za umma; na ujenzi wa miundombinu bora kwa lengo la kujenga uchumi wa viwanda chini ya Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano.
Taarifa kutoka Ikulu: Rais Magufuli ateua Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 27 Oktoba, 2016 amemteua Bw. Samwel Peter Kamanga kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC).
Bw. Samwel Peter Kamanga ameteuliwa kushika wadhifa huo kuanzia tarehe 27 Oktoba, 2016.
Kabla ya uteuzi huo, Bw. Samwel Peter Kamanga alikuwa akikaimu nafasi hiyo.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
Thursday, October 27, 2016
Mix Mtangazaji wa TV amempa ofa Obama kwenda Kenya… Lakini kwa sharti hili
Akiwa amebakiza siku chache kuendelea kuitawala nchi ya Marekani kama Rais wa nchi hiyo, Barack Obama amepewa ofa ya kushangaza na mtangazaji maarufu wa radio and TV aitwaye Sean Hannity, ambaye ni rafiki wa karibu wa mgombea Urais wa chama cha Republican Donald Trump.
Eti mwanamke kunyonywa matiti na mwanaume inapunguza maambukizi ya kansa?
Moja ya headline ambazo zimechukua nafasi kwenye mitandao ya kijamii ni pamoja na taarifa kwamba tafiti zinaonyesha kuwa mwanamke akinyonywa matiti na mwanaume inampunguzia kasi ya maambukizi ya ugonjwa wa kansa, wengine wameenda mbali zaidi na kusema itafika time wanawake wataanza kuwalipa wanaume pesa ilitu wawasaidie kuwanyonya matiti.
Millardayo.com imempata Naibu Waziri wa Afya, ustawi wa jamii, jinsia, wazee na watoto Hamisi Kigwangalla ambaye anasema kuwa sio kweli na ni upotoshwaji unafanyika.
‘Tafiti za tiba ni mama kumnyonyesha mtoto wake kwa miezi 12 na zaidi wala sio huko wanakozungumzia kwenye mitandao, kitaalamu ukinyonyesha mtoto kwa zaidi ya miezi 12 unapunguza kiwango cha uambukizo wa saratani ya matiti kwa asilimia 64‘ –Waziri Kigwangalla
‘Nimeona watu wanasema kuna wakati wanawake watakuwa wakiwalipa wanaume ili wawanyonye matiti huo ni upotoshwaji, wanachotakiwa kukijua ni kufuata misingi ya malezi kwa watoto ikiwa ni pamoja na kuwanyonyesha watoto wao kwa wakati‘ –Waziri Kigwangalla
Burudani AY kataja sababu ya kuacha kuwasimamia Stereo na Ommy Dimpoz….
Ni Headlines za Ambwene Yessaya aka AY ambae leo October 27, 2016 amefunguka na kusema sababu ya kuacha kusimamia Wasanii kama Stereo na wengineo.
Akiongea na millardayo.com & Ayo TV ameyasema haya>>>Hapana niliacha kwasababu kuna biashara zangu zingine ninazozifanya kama kuandaa vipindi vya Mkasi halafu sitaki kumdanganya mtu kwamba ninamsimamia lakini bado ninawasimamia mawazo ya hapa na pale, baada ya Ommy Dimopoz akafuata Stereo ndio wasanii ambao nilikuwa ninawasimamia’
UJAMBAZI WAKUTISHA DAR,WAFUNGA MTAA KWA SAA MBILI
NI ujambazi wa kutisha. Ndivyo unavyoweza kusema kutokana na kuibuka na wizi unaofanywa na majambazi katika maeneo mbalimbali nchini.Hatua hiyo inatokana na majambazi hao kuibuka na mbinu mpya kila kukicha katika matukio mbalimbali ambayo sasa yamekuwa yakishika kasi.
Mbali na mbinu ya kutumia pikipiki, majambazi hayo pia huvamia vibanda vya kutoa huduma za fedha, kuiba magari na hata wakati mwingine kuua.
Katika hali iliyovuta hisia za watu wengi, juzi usiku majambazi yalifunga mtaa kwa saa mbili na kupora fedha kwa watoa huduma ya fedha kwa njia ya simu katika eneo la Tabata jijini Dar es Salaam.
Mbali na maduka, watu wengine waliokuwa nje nao pia waliporwa simu na fedha. Hata hivyo thamani ya fedha na vitu vilivyoporwa havikujulikana mara moja.
Tukio hilo lililoshtua wakazi wengi wa mitaa ya Kimanga na Kisukuru wilayani Ilala, Dar es Salaam, ni la pili kutokea ndani ya kipindi cha mwezi mmoja.
Awali mwezi uliopita, majambazi wenye silaha walimuua kwa risasi askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na baadaye kumpora fedha Sh milioni tano, nje ya geti la nyumbani kwake Mtaa wa Kimanga, saa tano asubuhi.
Tukio la juzi lilitokea katika moja ya maduka yaliyoko pembezoni mwa kituo cha daladala cha Jiandae kilichopo Tabata Kimanga, ambako majambazi wanaokadiriwa kuwa zaidi ya wanne yaliingia dukani na kuwaamuru wafanyakazi kutoa fedha zote za mauzo ya siku, huku wakiwatishia kwa mapanga na bastola.
Mmoja wa wafanyakazi wa kike katika maduka hayo alipoteza fahamu baada ya tukio hilo na alikimbizwa hospitali kwa matibabu.
Licha ya idadi kubwa ya watu katika eneo hilo lenye biashara mbalimbali wakati wa jioni, majambazi hao hawakujali, walifanya uporaji huo na baadaye kutokomea kwa kutumia pikipiki aina ya Boxer.
Mashuhuda wa tukio hilo waliliambia MTANZANIA jana kuwa kwa muda wa dakika tano hakuna gari iliyoruhusiwa kwenda au kutoka Kimanga.
“Majambazi waliwaamuru wenye magari kutokukatiza eneo hilo, huku waenda kwa miguu wakiamriwa kuondoka haraka.
“Katika hali ya kawaida ni vigumu kuamini kama majambazi wanaweza kuvamia na kupora vitu katika maduka matatu kwa mpigo halafu wakatoweka bila kukamatwa,” alisema shuhuda huyo aliyekataa kutajwa jina.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kimanga, Manase Mjema, alipoulizwa kuhusu tukio hilo, alisema majambazi hao yalikuwa yamejiandaa na yalitumia silaha kubwa.
“Awali kabla ya kufyatua risasi yaliwaamuru wafanyakazi wa maduka yanayofanya biashara kupitia miamala ya simu kutoa fedha zote za mauzo, vijana walikuwa ngangari kidogo, hivyo majambazi waliamua kupiga risasi tatu hewani ndipo waliamua kutoa fedha walizokuwa nazo,” alisema.
Hata hivyo, mwenyekiti huyo alikiri kuwapo kwa ulinzi hafifu katika mtaa wake, huku pia akishauri Jeshi la Polisi kuimarisha doria mitaani kwa kuongeza askari wasiokuwa na sare ili wasitambulike kwa urahisi.
“Nikiri kwamba ulinzi wetu wa mtaa wakati wa usiku bado ni mdogo, tunaomba polisi nao waangalie mbinu mbadala za kukabiliana na uhalifu, na hasa ujambazi huu wa kutumia silaha za moto. Eneo la Tabata hivi sasa limekumbwa na matukio mengi ya ujambazi, kwa hiyo lazima mbinu nazo zibadilike,” alisema Mjema ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kimanga (Chadema).
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Lucas Mkondya, alikiri kupokea taarifa za ujambazi na tayari askari wake wameanza uchunguzi ili kuwabaini wahalifu hao.
“Nitoe ombi na nisisitize wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ili kutokomeza vitendo vyote vya uhalifu. Viongozi wote wa mitaa watupatie taarifa za watu wanaowatilia shaka, nasi tutazifanyia kazi,” alisema Kamanda Mkondya.
Katika siku za hivi karibu kumeibuka matukio ya ujambazi katika maeneo mbalimbali nchini huku wakiibua mbinu mpya za kufanikisha wizi huo.
Kutokana na hali hiyo majambazi hao wamekuwa wakitumia pikipiki kwa ajili ya kutekeleza uvamizi kwenye matukio hayo na hata wakati mwingine kuua watu na kujeruhi.
Katika mfululizo wa matukio ya ujambazi jijini Dar es Salaam, Agosti 23, mwaka huu, askari wanne wa Jeshi la Polisi waliuawa baada ya majambazi kuvamia Tawi la Benki ya CRDB lililopo Mbande, wilayani Temeke.
Majambazi hao wanaokadiriwa kufikia 14, wakati askari hao wakibadilishana lindo, waliibuka ghafla na kuanza kurusha risasi na askari mmoja aliyekuwa lindo alifanikiwa kukimbia.
Kutokana na foleni katika barabara nyingi za Dar es Salaam pamoja na miundombinu ya makazi yasiyokuwa rasmi, matukio mengi ya ujambazi yanayoripotiwa ni ya kutumia pikipiki, hivyo kuwapa wakati mgumu polisi ambao mara nyingi wanatumia magari ya doria.
Mapema mwaka huu Rais Dk. John Magufuli aliliagiza Jeshi la Polisi kutumia mbinu za kisasa katika kukabiliana na uhalifu na kuifanya nchi kuwa sehemu salama nyakati zote.
Dk Magufuli alionesha kushangazwa na askari wa Jeshi la Polisi kunyang’anywa silaha yake na majambazi na wakati mwingine kuuliwa na majambazi, akihoji uwezo wa majambazi kiasi cha kuwatesa polisi kiasi hicho.
Rais alikuwa akizindua Mpango wa kuboresha usalama wa jamii na mali zao, ambao una dhamira ya kupunguza uhalifu ambapo ameliagiza jeshi hilo kuwahi kushughulikia majambazi kabla ya wenyewe kushughulikiwa na majambazi hayo.
Pamoja na hali hiyo Jeshi la Polisi lilitangaza mikakati mbalimbali ikiwamo ukaguzi maalumu wa bodaboda na kufunga kamera za CCTV katika miji mikuu ili kufuatilia matukio mbalimbali.
Majambazi hao ambao kwa muda sasa wamekuwa wakiibuka na mbinu mpya ikiwamo ya kutumia bodaboda kuvamia benki na wanaotoka benki na kuwapora fedha.
Licha ya polisi kuweka ulinzi maalumu na waendesha bodaboda watakaoonekana kupakia kitu chochote na kukiweka mbele (katika tenki la mafuta) au kiti cha nyuma, ikiwemo kusimamishwa na kupekuliwa lakini bado mbinu hiyo imekuwa ikifeli na watu wakijikuta wakidhurika.
Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na matukio ya mara kwa mara ya wananchi kuvamiwa na kuporwa fedha, ikiwa ni muda mfupi baada ya kuzichukua benki huku wafanyakazi wa benki wakidaiwa kuhusika kutoa taarifa za wateja.
Mara zote majambazi hutumia bodaboda kufanikisha uhalifu huo, huku wakiwa na silaha ambazo huzitumia kutishia, kujeruhi na wakati mwingine kuua.
Chanzo: Mtanzania
BREAKING NEWS:HAYA HAPA MATOKEO YA MTIHANI DARASA LA SABA(7)2016
Serikali imetangaza matokeo ya mtihani wa darasa la 7 kwa mwaka 2016 ambapo ufaulu umeongezeka kwa asilimia 2.52 na shule iliyoongoza kitaifa ni shule ya Msingi Kwema ya mkoani Shinyanga
Kutokana na ukweli kwamba si kila mtu mwenye acces na mtandao na itambidi kwenda internet cafe kuangalia,MASWAYETU BLOG tumekurahisishia mambo.
Endapo utahitaji huduma ya kuangaliziwa jina la mwanao au ndugu yako fanya yafuatayo;
1.Tuma jina la mwanao,mkoa,wilaya na shule aliyosoma
(mfano:juma paul-PWANI,KIBAHA,UHURU PRIMARY)
kwenda namba 0652740927
2.Huduma hii uatozwa tshs 1000 tu.(kwa ajili ya kuisuport maswayetu blog)
3.Tuma pesa kwenda namba 0768260834-MPESA
0652740927-TIGO PESA
5.Utajibiwa ndani ya dk.moja tu,tuma pesa kwanza ndio ujibiwe
====>>BOFYA << HAPA>> KUTYAONA MATOKEO
AU
===> UNAWEZA BOFYA <> KUYAONA
Wednesday, October 19, 2016
Obama amtaka Trump kuacha kulalama kwamba anafanyiwa hila
Rais Barack Obama wa Marekani amemshutumu mgombea Urais nchini humo kupitia chama cha Republican Donald Trump kwa madai anayotoa kwamba kuna hila dhidi yake zinazofanywa katika uchaguzi nchini humo, na kumtaka kuacha kulalama.
Amesema malalamiko ya mgombea huyo ni jambo ambalo halijawahi kutokea kwa mgombea nchini Marekani kujaribu kutilia shaka uchaguzi hata kabla haujafanyika.
'' Sijawahi kuona katika maisha yangu ama katika historia za siasa za sasa kwa mgombea yoyote wa kiti cha Urais kujaribu kujaribu kutilia shaka uchaguzi na taratibu za uchaguzi kabla ya zoezi la upigaji kura kufanyika. Na hakuna ukweli wowote'' alisema Rais Obama.
Aidha Rais Obama amempa ushauri Mgombea huyo wa Republican ambaye ni mfanyabiashara tajiri Donald Trump kuendelea na kile anachokitafuta kuwa Rais ajaye wa Marekani.
''...Namshauri Bwana Trump kuacha kulalamika na kujaribu kuchukulia suala lake hilo kujaribu kupata kura. Na kama atapata kura nyingi hivyo itakuwa matarajio yangu kwa Hilary Clinton kutoa hotuba na kutaka kufanya naye kazi kwa ajili ya juhakikisha kwamba watu wa Matrekani wananufaika na serikali. Na itakuwa ni kazi yangu kumkaruibisha Bwana Trump bila kujali alichosema kuhusu mimi ama tofauti yangu dhidi yake juu ya mawazi yangu na pia kumsindikiza kuweza kukabidhiana madaraka kwa amani. Hivyo ndivyo Wamarekani wanavyofanya...'' Alisema Rais Obama
Rais wa Marekani pia amemlaumu Bwana Trump kuonesha kwake kumsifu Rais wa Urusi Vladmir Putin na sera zake kufuata za kiongozi huyo.
Kampeni za Uchaguzi nchini Marekani zimekuwa zikifanyika katika hatua za lala salama, ikiwa imebaki siku chahe kufanyika kwake. huku Donald Trump akiendelea kuwaambia wafuasi wake kwamba serikali ya nchi hiyo, imekuwa ikimchafua lakini atashinda.
Moto wateketeza Mabweni 2 ya Shule ya Kondoa Islamic
Moto wateketeza Mabweni mawili ya wasichana ya Shule ya Sekondari ya Kondoa Islamic iliyopo Kondoa Mjini, Moto huo ulianza majira ya saa 3 usiku kuamkia leo na kusababisha taharuku kubwa kwa wanafunzi na wazazi kwa ujumla ndipo juhudi za kuuzima Moto huo zikaanza na kuweza kuafanikiwa kuuzima moto huo majira ya saa 5 usiku.
Hata hivyo kamati ya ulinzi na salama ya Wilaya ilifika hapo shuleni na kujionea uharibifu huo, mpaka sasa haijafahamika chanzo cha Moto huo na hasara kwa ujumla.
Vyeti vya Mwigulu vyaibua utata
Wakati Serikali ikitanfaza msako kwa watu walioghushi vyeti na kutumia majina ya watu wengine, Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi, Mwigilu Nchemba, ameibuka na kutoa ufafanuzi wa utata wa majina yake.
Hatua hiyo imekuja baada ya kuibuka kwa mjadala wa usahihi wa majina yake pamoja na kuhusishwa kughushi vyeti ya elimu.
Katika andiko lake aliloliweka jana katika mitandao ya kijamii ambalo baadaye lilithibitishwa na mmoja wa wasaidizi wake, Mwigulu alisema watu wanaoandika historia yake hawamjui kwani uhalisia alikuwa akiitwa Lameck Madelu Mkumbo, sasa Lameck si jina la Kinyiramba na Madelu si jina halisi la baba yake bali la utani.
“Ni vema kuweka rekodi sawa, kwanza anasema (aliyeandika) nilikuwa naitwa Lameck Madelu Mkumbo, sasa moja Lameck sio jina la kinyiramba, na Madelu sio jina halisi la baba bali ni utani kuwa ana ndevu nyingi, yaani ni mandevu. Ndiyo maana hata kwenye ubunge nililiongeza tu kama a.k.a ili watu, hasa wazee wanifahamu, hili haliko kwenye vyeti.
“Hili la Lameck siyo jina la Kinyiramba ni jina la daktari aliyenipokea zahanati iliyopo Kijiji cha Mukulu, daktari tunaita hivyo, lakini ni nesi ndiye aliyekuwa anaitwa Mwigulu na jina la kizungu Lameck.
“Mimi nilipelekwa hospitali nikiitwa Mugulo na jina la ukoo kwa watoto wote wa kiume ni Shumbi, ambalo hata hivyo wanatumia wazee tu, wanaojua Kinyiramba hilo ndio jina la Kinyiramba,” alisema Mwigulu na kuongeza:
“Mama yangu aliulizwa jina akanitaja kwa muuguzi (nesi) akamwambia mama unamwitaje jina hilo hakuna lingine, mama akamwambia hakuna labda mtaje wewe, basi jamaa akajitaja,” alisema.
Alisema suala hilo ni jambo la kawadai hasa kwa kijijini kwani familia inakuwa na watoto wengi hadi majina inakuwa si jambo la kujali.
“Hata pale kijijini kuna wengine waliotajwa majina ya waganga wa kienyeji wazee walikopewa dawa, majina ya manesi, matabibu kama mimi, majina ya walimu,” alisema.
Akizungumzia maisha yake ya elimu, alisema aliacha shule kwa mara ya kwanza mwaka 1984 baada ya kuanza na kaka yake aliyemtaja kwa jina la Jugulu.
Mbunge huyo wa Iramba alisema kutokana na hali hiyo, baba yao aliwataka wapeane zamu ya kwenda shule hali iliyomfanya aache shule.
“Mwaka 1985, nikaachia darasa la tano nikaenda kuchunga miaka kama miwili. Nikarudi tena baada ya mifugo kuanza kufa sana, mzee akashauriwa awekeze kwenye elimu. Walimu walikuwa wanashinda nyumbani kumsihi anirudishe shule, ndiyo nikarudi na nikachukua majina ya daktari.
“Mtu asichanganye kuona ni udanganyifu, mimi sijachukua vyeti vya mtu. Nimefanya mitihani tena kwa kupiga na picha za passport ili mtu asitumie haki ya mtu mwingine aliyefaulu na mpaka sasa naona ni struggle (kupambana) za mfano, kuwa nilisoma kwa mazingira ya kutoka kuchunga na kurudishwa shule na kufaulu mwenyewe,” alisema Mwigulu.
Waziri huyo alisema kwa anayetaka kuthibitisha maelezo aliyotoa, anaweza kuwauliza aliosoma nao shule ya msingi.
“Comrades kwa mawazo yangu kosa ni mtu kuchukua nafasi ya mtu aliyefaulu na kwenda yeye, hapo ni kuiba haki ya mtu. Najua hii ilikuwa ikitokea baadhi ya maeneo, mtu anafaulu ila anakuwa hataki kwenda shule au amefariki then anakwenda mwingine. Mimi sijawahi chukua nafasi ya mtu.
“Halafu watu wanasema jina la mtu, labda kama wanamaanisha tofauti na wizi wa jina kwani kila mmoja hapo alipo ana jina la mtu, yaani atakuwa John wa Biblia, Mohamed wa Quran, litakuwa la babu, bibi la mganga, daktari, rafiki, kiongozi au hata la tukio.
“Nijuavyo jina unakula kiapo tu kama sio la kwako kisheria na unatumia, na hata sasa nikitamani jina jipya nakula kiapo na kutangaza katika Gazeti la Serikali na lisipopingwa ndiyo linakuwa jina langu jipya.
“Hoja ni kama mtu kapora cheti cha mtu, kapora nafasi ya mtu mwingine aliyefaulu akaenda kuisomea yeye. But, things do change pia kutokana na nyakati na mazingira,” alisema Mwigulu.
Source: Mtanzania
MWANZA: Maduka 70 yamefungwa na halmashauri ya Jiji
Takribani maduka 70 yaliyopo kandokando ya Shule ya Sekondari Pamba yaamefungwa na halmashauri ya jiji kwa tuhuma za wafanyabiashara hao kukwepa kodi. Displaying jamiiforums-20161019-0001.jpg
Hatua ya kuyafunga Maduka hayo imelenga kukusanya shilingi bilioni 2 kwa mwaka katika vyumba vya wafanyabiashara wa jiji la Mwanza.
Halmashauri ya jiji la Mwanza inamiliki jumla ya vyumba vya Maduka 1024.
Chanzo: JamiiForum
Leicester City yang'ara UEFA
Klabu ya soka ya Leicester City imeendeleza wimbi la ushindi katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya FC Copenhagen.
Wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani King Power, Leicester walipata bao hilo dakika tano kabla ya kwenda mapumzikoni kupitia kwa Riyad Mahrez aliyekuwa katika kiwango cha hali ya juu baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Mualgeria mwenzake Islam Slimani.
Islam Slimani alikataliwa bao baada ya kuotea
Kwa matokeo hayo Leicester wanabaki kileleni mwa kundi G wakiwa na alama 9 baada ya kushinda michezo yote mitatu ya ufnguzi wa ligi ya mabingwa Ulaya.
Timu pekee zilizowahi kushinda michezo mitatu ya ufunguzi katika michuano hiyo ni AC Milan, Paris St-Germain, Juventus na Malaga.
Matokeo mengine ya Ligi ya mabingwa barani Ulaya
Bayer 04 Leverkusen 0-0 Tottenham Hotspur F.C.
CSKA Moscow 1-1 AS Monaco FC
Real Madrid 5-1 Legia Warsaw
Sporting 1 -2 Borussia Dortmund
Club Brugge 1-2 FC Porto
Dinamo Zagreb 0- 1 Sevilla
Lyon 0- 1 Juventus
Tamko la Serikali kuhusu Viza ya pamoja katika nchi za Afrika Mashariki
http://i2.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2016/10/NJE.png?resize=640%2C362
Baada ya kuripotiwa kuwa Serikali ya Tanzania imejiondoa kwenye mchakato wa kuwa na Viza moja itakayotumika kwa masuala ya utalii katika nchi zote za Afrika Mashariki, Wizara ya Mambo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imetoa tamko kuhusiana na taarifa hizo.
Serikali imesema suala la uanzishwaji wa Viza ya pamoja ya Afrika Mashariki bado liko kwenye majadiliano ya nchi wanachama kupitia vikao vya Sekta ya Utalii na Wanyamapori, na katika kufanikisha kusudio hilo Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Usimamizi wa Wanyamapori uliofanyika November 1, 2008 liliunda kikosi kazi kwaajili ya kufanya utafiti kwa lengo la kubainisha mahitaji na utayari wa nchi wanachama.
Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeeleza kuwa katika vikao vilivyofanyika mwaka 2010 kulikua na masuala muhimu ambayo yanatakiwa kuzingatiwa kabla ya kuanzisha kwa Viza ya pamoja ya Utalii. Millardayo.com inakuletea mambo 6 yaliyobainishwa kwenye mkutano huo.
Kurazinisha (Harmonization) sheria za Viza za Nchi Wanachama.
Idara ya Uhamiaji kuanzisha Mfumo wa kudhibiti Usalama.
Utoaji wa Viza kuwa wa Kielektroniki.
Kuwepo kwa mfumo wa ukusanyaji na ugawanyaji wa mapato pamoja na namna ya kuyalipa.
Kuwepo kwa maafisa uhamiaji katika ofisi za ubalozi.
Kujenga uwezo wa watumishi kwenye suala la mfumo wa kielektroniki wa utoaji Viza ya pamoja.
Kufuatia matokeo ya utafiti huo, mkutano wa 5 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Utalii na Usimamizi wa Wanyamapori uliofanyika Julai 2013 jijini Bujumbura Burundi uliagiza kuundwa kwa kamati itakayojumuisha wataalamu kutoka Taasisi za Uhamiaji, Utalii, Fedha, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Tehama, Usalama na Sheria katika nchi wanachama ili kuandaa mpango kazi na kushughulikia mambo yote ya uanzushwaji wa Viza hiyo.
Hata hivyo kabla ya utekelezaji wa maagizo hayo, nchi za Uganda, Kenya na Rwanda zilianzisha Viza ya pamoja ya Utalii kwenye nchi zao ikiwa ni nje ya vikao vya jumuiya.
Taarifa ya Benard Haule ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Biashara Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeeleza kuhusu tamko hili.
.
MH.ANTONY MTAKA ATEKELEZA AHADI YA MH.MAGUFULI YA VIWANDA KWA VITENDO MKOANI SIMIYU
http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/3421942/highRes/1466147/-/maxw/600/-/109k4x0z/-/Mtaka.jpg
Baada ya Mkoa wa Simiyu kukamilisha uanzishwaji wa viwanda vidogovidogo kwenye wilaya za Meatu na Maswa, hivi sasa umeanza kazi hiyo kwa Itilima, Bariadi na Busega ili kwenda sambamba na uamuzi wa Rais John Magufuli.
Wilaya ya Meatu imeanzisha Kiwanda cha Kusindika Maziwa, huku Maswa ikianzisha Kiwanda cha Uzalishaji Chaki vyote vikishirikisha makundi ya vijana.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka alisema Bariadi inatarajiwa kuanzisha kiwanda cha kutengeneza sabuni; Busega kitajengwa kiwanda cha maji wakati mipango zaidi ikiendelea kuangalia kiwanda kinachofaa wilayani Itilima.
Mtaka alisema katika kutekeleza azma ya Tanzania ya viwanda, mkoa umekuwa ukifanya jitihada za kuwaunganisha vijana kwa kuwajengea uwezo wa kujitegemea.
“Ni fedheha kuona hata bandeji za hospitalini zinatoka nje huku malighafi zake inapatikana nchini. Ni vyema kuzitumia fursa zilizopo na mikakati ya kuanzisha kiwanda cha bandeji na maji,” alisema Mtaka.
Katika kutekeleza kaulimbiu ya mkoa huo ya ‘One district one product’, wanatarajia kuwashirikisha vijana na kuwajengea uwezo ili wafanye kazi za kujiletea maendeleo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu), Jenista Mhagama alisema wizara yake itaendelea kuwaunga mkono vijana wanaothubutu kwa kuwapa mikopo ili waazishe miradi.
Mhagama alisema vijana wa Simiyu wameonyesha njia kwa wenzao nchini na kuwaahidi kuwapa mkopo wa Sh30 kwa kuanzisha kiwanda cha chaki na maziwa.
Aliwataka vijana kuchangamkia fursa badala ya kukaa vijiweni na kulalamika kuwa hawana kazi.
mkopo wa elimu ya juu
FOLLOW OFFICIAL MASWAYETU BLOG INSTAGRAM NOW ,KUPATA HABARI KILA SEKUNDE ZINAPOTOKEA BONYEZA HAPA FOLLOW
Mikopo bilioni 80/- elimu ya juu yapelekwa vyuoni kwa ajili ya first years 2016/2017
Paun Jotia 09:13:00 No comments
[IMG]
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Mafunzo ya Ufund, Stella Manyanya.
SERIKALI imetoa Sh bilioni 80 kwa ajili ya malipo ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu wanaoanza na wanaoendelea na masomo na wameanza kulipwa jana.
Aidha, imewataka wakuu wa vyuo ambao hawajawasilisha matokeo ya wanafunzi wao wanaoendelea na masomo kufanya hivyo haraka ili wakamilishe uchakataji wa mgawo wa mikopo. Katika mwaka huu wa fedha, serikali imetenga Sh bilioni 427 kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Stella Manyanya alisema hayo Dar es Salaam jana wakati akielezea mchakato wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na kueleza kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya wanaoanza na wanaoendelea katika robo mwaka.
Manyanya alisema serikali imetoa fedha zinazotakiwa kukamilisha mchakato wa malipo unaofanyika kuanzia jana baada ya kumalizika kwa uchambuzi kulingana na vigezo.
Alisema kwa mujibu wa ulipaji mikopo, inazingatiwa vigezo vya kisheria vya kutoa mikopo kulingana na uhitaji kwa kuangalia anayepewa, kweli ana uhitaji na siyo kwa kila mtu kwani lengo la serikali kusaidia na siyo kuondoa majukumu ya mzazi.
Alisema pia wanaangalia bajeti iliyopo kwa wakati huo, kwani kwa mujibu wa Sera ya Elimu ya Mwaka 2014 na matamko ya Rais John Magufuli amedhamiria kuendelea kutoa mikopo kwa wahitaji wote pamoja na kuboresha elimu kwa namna mbalimbali.
Alitaja baadhi ya miradi iliyotekelezwa sambamba na kutoa mikopo ni ukamilishaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Mloganzila kwa Sh bilioni 100 pamoja na kukamilisha ukarabati wa vyuo vya ualimu ambapo tayari vyuo 10 vimekamilika.
Alisema pia baada ya Rais kutembelea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na kuona adha ya wanafunzi kukabiliwa na kukaa mbali na chuo, Sh bilioni 10 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa mabweni 20 katika ghorofa tatu zitakazochukua wanafunzi 3,800.
Manyanya alisema pia serikali imelipia ada moja kwa moja vyuoni kwa wanufaika wa mikopo ya Sh bilioni 40 katika vyuo vya serikali na binafsi nchini.
Aliwataka wanafunzi wanaolalamika kutopata mikopo kukamilisha kupeleka viambatanisho vyote stahili huku wakihakikisha wanakuwa na vigezo vya ufaulu kwani sasa ufaulu umepanda wengi wamepata daraja la kwanza na pili, hivyo kuchukua hao kwanza na wale wa daraja la tatu wachache.
Naibu Waziri alisema kwa yatima wapo wasiopewa mikopo baada ya uchambuzi kubaini kuwa na uwezo wa kujilipia kutoka kwa ndugu au mali zilizoachwa na wazazi hivyo kuna utofauti wa yatima, kwani wapo wahitaji na wasio wahitaji.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Abdul Razaq Badru alisema bodi hiyo hutoa mikopo kwa kuzingatia kozi za vipaumbele kama udaktari au uhandisi kwa ajili ya ujenzi wa wataalamu katika Tanzania ya viwanda.
Alisema pia mikopo hutolewa kwa ulinganifu wa uhitaji kwa asilimia huku wakifanya uchambuzi wa kina ili kuwafikia wahitaji wengi na wanufaika kuongezeka kama anavyotaka rais.
Katika hatua nyingine, Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu (Tahliso) imesema kuwa muongozo mpya wa utoaji mikopo uliotolewa kwa mwaka huu wa masomo 2016/17 utawahusu wadahiliwa wapya tu wanaoanza masomo.
Taarifa iliyotolewa jana na Tahliso kwenda kwa wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu, ilieleza kuwa wanafunzi wanaonufaika na mikopo ambao wanaendelea na masomo, wao wataendelea na utaratibu kama ulivyokuwa tangu awali walivyoingia makubaliano na utaratibu mpya hautawaathiri.
Mwenyekiti wa Tahliso, Stanslaus Kadugalize ambaye amesaini taarifa hiyo, alifafanua kuwa msimamo huo umetolewa baada ya jumuiya hiyo kuingilia kati baada ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi kutoa mwongozo wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.
Kadugalize alisema baada ya kutolewa kwa mwongozo huo walienda kufanya majadiliano na Waziri, Profesa Joyce Ndalichako ili kumwomba wabadili msimamo wa mwongozo huo kwa kuwa utawaathiri wanafunzi wengi ambao ni watoto wa maskini.
Hivi karibuni Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia walitangaza vigezo vya utoaji mikopo kuwa kuanzia mwaka huu wa masomo, wanufaika wote wa mikopo wapya na wanaoendelea na masomo watakopeshwa kulingana na uwezo wao (means tested) katika vipengele vyote vya mikopo.
Tahliso ilieleza kuwa kutokana na maelezo hayo ni dhahiri mikopo kwa wanafunzi wanaoendelea hasa kwa wale wenye wazazi bila kujali ana uwezo ama hana uwezo, mikopo yao ingepungua kutoka kwenye asilimia walizopangiwa awali.
Taarifa hiyo ilisisitiza kuwa muongozo huo ungepelekea fedha inayotolewa kwa ajili ya chakula na malazi kupungua, jambo ambalo lingesababisha wanafunzi wengi kushindwa kuendelea na masomo, kutokana na uwezo wa wafamilia wanazotoka hasa watoto wa maskini ambao hutegemea fedha hizo hizo za boom kulipia sehemu ya ada iliyobakia na huku wakiendelea kuishi maisha ya shida vyuoni.
Katika vigezo hivyo, Serikali ilisema itatoa kipaumbele kwanza kwa wanafunzi wanaoenda kusomea fani za Sayansi za Tiba na Afya, Ualimu wa Sayansi na Hisabati, Uhandisi wa Viwanda, Kilimo, Mifugo, Mafuta na Gesi Asilia, Sayansi Asilia na Mabadiliko ya Tabianchi na wale watakaosomea Sayansi za Ardhi, Usanifu Majengo na Miundombinu.
Kwenye vigezo hivyo pia serikali ilisisitiza kuwa kipaumbele kingine kitakuwa ni kwa waombaji hususani wenye mahitaji maalumu kama vile ulemavu na yatima.
Seebait.com 2016SeeBait
BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APPLICATION MPYA YA MASWAYETU BLOG
Share:
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook
Related Posts:
HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA STEFFANO MOSHI MEMORIAL UNIVERSITY 2016/2017
TANGAZO MAALUM KWA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA BUGANDO-CUHAS MWANZA 2016/2017
TAARIFA MUHIMU KUTOKA BODI YA MIKOPO KUHUSU UHAKIKI WA WANAFUNZI UNAFANYIKA UDSM KUANZIA TAREHE 27-29 SEPTEMBA, 2016
MPYA:GAS NA MAJIKO YANAUZWA KWA BEI NAFUU KABISA,UNALETEWA HADI MLANGONI KWAKO
MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO KIKUU SEBASTIAN KOLOWA-SEKOMU DIGRII/BACHELOR 2016/2017
← Newer Post Older Post → Home
Post a Comment
Popular Posts
MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017
Kama kawaida yetu MASWAYETU BLOG katika nusanusa yetu tumefanikiwa kunasa hii ambayo ilikuwa ikisubiriwa na watu wengi,ni kuhusu ...
UPDATED:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA SELECTION YA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017
Habari yako, Maswayetu blog,tumedhamiria kuwapa vitu roho inapenda hapa mjini,Tumeamua kukuwekea list ya vyuo vikuu ambavyo vimetoa m...
MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI 10,027 WALIOKOSEA KUJAZA FORM ZA MIKOPO BODI YA MIKOPO 2016/2017
KUONA MAJINA HAYO << BONYEZA HAPA--PDF >>
MPYA:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA SECOND ROUND VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017
Habari yako, Maswayetu blog,tumedhamiria kuwapa vitu roho inapenda hapa mjini,Tumeamua kukuwekea list ya vyuo vikuu ambavyo vimetoa ma...
MPYA:HAYA HAPA MAJINA (KATIKA PDF) WANAFUNZI SPECIAL DIPLOMA WALIOPANGIWA KURUDI UDOM &VYUO VINGINE 2016
>>> CLICK HERE FOR LIST OF SELECTED STUDENT - UDOM (53.28 kB)<<< CLICK HERE FOR LIST OF SELECTED STUDENTS - TEACHER ...
ANGALIA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWAPAMOJA NA APPLICATIONS FOR ADMISSION INTO NON DEGREE (DIPLOMA AND CERTIFICATE) PROGRAMMES FOR ACADEMIC YEAR 2016/2017-NACTE
Nacte wametoa majina ya wanafunzi waliofanikiwa kuchaguliwa katika vyuo mbalimbali afya,ualimu ,kil...
BREAKING NEWS:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO MWAKA WA MASOMO 2016/2017-FIRST BATCH
Bodi ya mikopo ya elimu ya juu wametangaza majina ya wanafunzi waliopata mkopo 2016/2017 awamu ya kwanza. Kama utahitaji kuangaliziwa ...
MPYA:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA SECOND ROUND VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017
Habari yako, Maswayetu blog,tumedhamiria kuwapa vitu roho inapenda hapa mjini,Tumeamua kukuwekea list ya vyuo vikuu ambavyo vimetoa ma...
MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO KIKUU UDOM 2016/2017
<<>> BONYEZA HAPA KUONA MAJINA YA VYUO VINGINE ...
BREAKING NEWS:HIZI HAPA SIFA ZA KUJIUNGA NA CHUO KIKUU MWAKA WA MASOMO 2016/2017-TCU
Tanzania Commission for Universities PUBLIC NOTICE CHANGE OF PROCEDURES, REQUIREMENTS AND MINIMUM ADMISSION ENT...
Recent Posts
Text Widget
Pages
Home
Blog Archive
▼ 2016 (2265)
▼ October (180)
▼ Oct 19 (11)
MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA ...
MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA HOSTE...
MPYA:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA MAJINA YA WA...
Zitto Atoa Neno Ugomvi wa RC Arusha na Godbless Le...
MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA ...
MH.ANTONY MTAKA ATEKELEZA AHADI YA MH.MAGUFULI YA ...
Mikopo bilioni 80/- elimu ya juu yapelekwa vyuoni ...
MAGAZETI YA LEO JUMATANO OCTOBER 19 2016
Rais Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi Kufuatia ...
MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI MWAKA WA KWANZA...
Mwanafunzi apigwa Dar, ‘afa, afufuka’ mochwari
► Oct 18 (16)
► Oct 17 (7)
► Oct 16 (9)
► Oct 15 (2)
► Oct 14 (4)
► Oct 13 (5)
► Oct 12 (11)
► Oct 11 (8)
► Oct 10 (15)
► Oct 09 (10)
► Oct 08 (10)
► Oct 07 (17)
► Oct 06 (15)
► Oct 05 (14)
► Oct 04 (8)
► Oct 03 (11)
► Oct 02 (5)
► Oct 01 (2)
► September (286)
► August (251)
► July (233)
► June (260)
► May (309)
► April (210)
► March (233)
► February (264)
► January (39)
► 2015 (1416)
► 2014 (1348)
ONLINE VISTORS
450 ONLINE
Mikopo bilioni 80/- elimu ya juu yapelekwa vyuoni kwa ajili ya first years 2016/2017
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Mafunzo ya Ufund, Stella Manyanya.
SERIKALI imetoa Sh bilioni 80 kwa ajili ya malipo ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu wanaoanza na wanaoendelea na masomo na wameanza kulipwa jana.
Aidha, imewataka wakuu wa vyuo ambao hawajawasilisha matokeo ya wanafunzi wao wanaoendelea na masomo kufanya hivyo haraka ili wakamilishe uchakataji wa mgawo wa mikopo. Katika mwaka huu wa fedha, serikali imetenga Sh bilioni 427 kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Stella Manyanya alisema hayo Dar es Salaam jana wakati akielezea mchakato wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na kueleza kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya wanaoanza na wanaoendelea katika robo mwaka.
Manyanya alisema serikali imetoa fedha zinazotakiwa kukamilisha mchakato wa malipo unaofanyika kuanzia jana baada ya kumalizika kwa uchambuzi kulingana na vigezo.
Alisema kwa mujibu wa ulipaji mikopo, inazingatiwa vigezo vya kisheria vya kutoa mikopo kulingana na uhitaji kwa kuangalia anayepewa, kweli ana uhitaji na siyo kwa kila mtu kwani lengo la serikali kusaidia na siyo kuondoa majukumu ya mzazi.
Alisema pia wanaangalia bajeti iliyopo kwa wakati huo, kwani kwa mujibu wa Sera ya Elimu ya Mwaka 2014 na matamko ya Rais John Magufuli amedhamiria kuendelea kutoa mikopo kwa wahitaji wote pamoja na kuboresha elimu kwa namna mbalimbali.
Alitaja baadhi ya miradi iliyotekelezwa sambamba na kutoa mikopo ni ukamilishaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Mloganzila kwa Sh bilioni 100 pamoja na kukamilisha ukarabati wa vyuo vya ualimu ambapo tayari vyuo 10 vimekamilika.
Alisema pia baada ya Rais kutembelea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na kuona adha ya wanafunzi kukabiliwa na kukaa mbali na chuo, Sh bilioni 10 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa mabweni 20 katika ghorofa tatu zitakazochukua wanafunzi 3,800.
Manyanya alisema pia serikali imelipia ada moja kwa moja vyuoni kwa wanufaika wa mikopo ya Sh bilioni 40 katika vyuo vya serikali na binafsi nchini.
Aliwataka wanafunzi wanaolalamika kutopata mikopo kukamilisha kupeleka viambatanisho vyote stahili huku wakihakikisha wanakuwa na vigezo vya ufaulu kwani sasa ufaulu umepanda wengi wamepata daraja la kwanza na pili, hivyo kuchukua hao kwanza na wale wa daraja la tatu wachache.
Naibu Waziri alisema kwa yatima wapo wasiopewa mikopo baada ya uchambuzi kubaini kuwa na uwezo wa kujilipia kutoka kwa ndugu au mali zilizoachwa na wazazi hivyo kuna utofauti wa yatima, kwani wapo wahitaji na wasio wahitaji.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Abdul Razaq Badru alisema bodi hiyo hutoa mikopo kwa kuzingatia
Zitto Atoa Neno Ugomvi wa RC Arusha na Godbless Lema
lema
Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameamua kutoa ya moyoni kufuatia hali iliyojitokeza jana mkoani Arusha wakati wa uzinduzi wa Hospitali ya Mama na Mtoto. Katika uzinduzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo alisema kuwa eneo la hospitali hiyo lilitolewa na familia ya Nyaga Mawalla,
jambo ambalo wananchi walilipinga wakishirikiana na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) na kuzua sintofahamu kama inavyoonekana katika video hii….
Zitto kupitia akaunti yake ya Facebook ameandika hivi; “Nakasirishwa sana kuona viongozi vijana wanafanya mambo ya hovyo. Mkuu wa Mkoa wa Arusha mdogo wangu Mrisho Gambo una dhamana zaidi Kwa vijana. Mnapofanya mambo ya kijinga mnaharibu nafasi ya vijana kuaminiwa zaidi. Kaa Na Mbunge Godbless Lema mnywe kahawa pale New Arusha Na muanze upya. Ndugu yangu Lema nashauri punguza munkari. Juhudi zako Arusha haziwezi kufutika kirahisi. Nakushauri kaa chini Na Mkuu wa Mkoa wako mpige mstari muanze Kazi upya Kwa pamoja.
Viongozi jiepusheni kuonyesha hasira zenu hadharani. Sio hekima.”
Tuesday, October 18, 2016
Kama wewe ni mtunzaji misitu au mazingira hii inaweza kukuhusu
http://i0.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2016/10/IMG-20161018-WA0022.jpg?resize=660%2C400
Kwa muda mrefu tumekuwa na kampeni nyingi za kuhamasishana kuhusu upandaji miti au utunzaji misitu na wapo baadhi ya watu wetu ambao walishawahi kufikiwa na zawadi kuhusiana na issue ya Mazingira kwenye list yako ya watu waliopata zawadi kutokana na mazingira inabidi uwaongeze wananchi wa Kijiji cha Katurukila Morogoro.
img-20161018-wa0020
Nimeipata ya Waziri wa Mazingira na Muungano ofisi ya Makamu wa Rais,January Makamba ameahidi kutoa mifuko 100 ya saruji kwa kijiji cha Katurukila wilaya ya Kilombero Morogoro, kama kutambua mchango wao mkubwa katika utunzaji wa mazingira hasa eneo la Msitu wa Magombera.
img-20161018-wa0026
Miongoni mwa maeneo ya Kilombero ambayo January Makamba ameyatembelea ni pamoja, Kilosa kwenye Mto Mkondoa, Kilombero, Msitu wa Magombera,Kijiji cha Kiturukila na Mto Lumemo Ifakara, kuhusu mgogoro wa msitu wa Magombera kati ya wanakijiji na mwekezaji Ramadhan Rashid Kuhuka, Waziri Makamba amesema kuwa tayari kesi imeshafika mahakamani na ni busara kuiachia mahakama.
Burudani Kinara wa bendi nchini Tanzania kuingia studio na Davido……
http://i0.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2016/10/DE324467555.jpg?resize=538%2C357
Ni headlines za mwimbaji wa bendi kutoka Akudo Impact, Taasisi Masela ambae kwasasa yupo katika maandalizi ya kutoa single zake ikiwemo matarajio ya kuwepo kwa collabo yake na msanii wa Nigeria Davido.
Mwimbaji huyo akiipata heshima millardayo.com & Ayo TV na kuyaongea haya..>>Kuhusu collabo yangu na Davido ndiyo ipo tulikutana congo wakati nilipoenda kusheherekea miaka 30 yangu na bahati nzuri Davido nilishawahi kusafiri nae kwenye ndege moja basi tukabadilisha mawasiliano yeye alikuwa akielekea London mimi naelekea Dubai
‘Kwahiyo basi mazungumzo yetu yalikuwa na marefu sana nikazungumza nae kuhusu collabo yangu na yeye akanimbia kwa kipindi hiki yuko busy sana tukapanga kuanzia mwakani itabidi niende Nigeria kukamilisha collabo hiyo’
Mix Maamuzi ya mahakama kuu kuhusu maombi ya Mbowe kurudishwa kwenye jengo la NHC
http://i1.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2016/10/NNN.jpg?resize=576%2C400
Hatima ya maombi ya mfanyabiashara na mwanasiasa, Freeman Mbowe kutaka kurudishwa kwenye jengo la Billcanas baada ya kuondolewa na shirika la nyumba la Taifa ‘NHC’ kwa kudaiwa kodi ya Bilioni 1.3 imejulikana leo baada ya mahakama kuu kitengo cha ardhi kufuatilia mbali maombi hayo.
Mix Makubaliano 4 yaliyopitishwa kwenye kikao kati ya Serikali ya DRC na upinzani
http://i2.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2016/10/KABILA.jpg?resize=660%2C400
Baada ya kuendelea hali ya machafuko na uvunjifu wa amani nchini Congo, hatimaye Serikali ya DRC imefanya kikao jana Jumatatu October 17, 2016 kati yake na upande wa Upinzani nchini humo na kupitisha makubaliano manne ikiwa ni njia mojawapo za kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wa kisiasa unaolisumbua taifa hilo kwa zaidi ya miaka 10.
Makubaliano hayo yamepitishwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kati ya vyama vinavyounga mkono serikali na baadhi ya vyama vya upinzani pamoja na baadhi ya mashirika ya kiraia. Kwa mjibu wa ripoti ya shirika la habari la AFP iliyotolewa na msuluhishi wa Umoja wa Afrika Edem Kodjo inaelezwa kuwa makubaliano hayo yanatazamiwa kusainiwa leo Jumanne October 18, 2016 mjini Kinshasa na watu 300 walioshiriki katika mazungumzo.
media
Makubaliano hayo yaliyopitishwa katika kikao cha Jumatatu Oktoba 17, 2016 ni kuitaka Serikali kutekeleza masuala yafuatayo.
1. Tarehe ya uchaguzi
Hoja ya kwanza ya makubaliano yaliyofikiwa na vyama vinavyounga mkono serikali na upinzani ni kutotajwa tarehe ya uchaguzi wa urais, wabunge na wawakilishi wa majimbo. Tarehe pekee iliyotajwa ni tarehe ya kuwasilisha fomu za kugombea ambayo ni October 30, 2017.
Uchaguzi mkuu utafanyika ndani ya muda wa miezi sita ambayo ni wishoni mwa mwezi Aprili 2018, ndivyo wajumbe wa vyama vinavyunga mkono serikali na upinzani walivyoafikiana. Ingawa baadhi ya wajumbe wamekua wakijiuliza kama Tume ya Uchaguzi itaheshimu tarehe hiyo mpya.
2. Waziri mkuu kutoka chama cha upinzani
Hoja ya pili, Waziri Mkuu atateuliwa kutoka katika chama cha upinzani kilichoshiriki katika mazungumzo. Hakuna maelezo kuhusu kugawana nyadhifa katika serikali ya umoja wa kitaifa na Serikali itaundwa ndani ya siku 21 baada ya kusainiwa mkataba.
3. Kamati ya ufuatiliaji
Hoja ya tatu, kamati ya ufuatiliaji itakutana mwezi mmoja baada ya kusainiwa kwa mkataba: wajumbe saba kutoka vyama vinavyounga mkono serikali, wengine saba kutoka vyama wa upinzani na watatu kutoka vyama vya kiraia.
4. Ukomo wa utawala wa Rais Joseph Kabila
Hoja ya nne, Kuhusu hatma ya rais Joseph Kabila baada ya Desemba 19, imeelezwa kuwa Rais huyo ataendelea kubakia madarakani hadi atakapoapishwa Rais mwengine. Makubaliano hayo yanazungumzia juu ya kuzingatia Katiba.
Hata hivyo vyama vya upinzani ambavyo vinajumuika katika muungano wa “Rassemblement” pamoja na baadhi ya mashirika ya kiraia ambayo yalisusia mazungumzo hayo yametoa wito wa kumiminika mitaani Jumatano Oktoba 19.
Wakati hayo yakijiri, Tume ya Uchaguzi ya Congo (CENI) imeruhusiwa na Mahakama ya Katiba kuahirisha rasmi uchaguzi mkuu wakati ambao hali ya wasiwasi na hofu ya kutokeamachafuko nchini DR Congo imeendelea kutanda
MPYA:TAARIFA KWA UMMA KUTOKA JESHI LA KUJENGA TAIFA JKT LEO TAREHE 17.10.2016
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhM1hfKDnjyz1wAyfVxNi_VDMQWEYPGVlUff2NNbbX7tadtB6Fdt2oS7VN07qhG_JTaCRIKEFcISr4Dh5zAC-gX63fC_MKsAnR8h3hhoZt56Xvs-N3eAy71LD0Kq9WFXPBDymxUy0EOfQY/s1600/index.jpeg
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga Afikishwa Mahakamani Kwa Kosa La Kumtishia Bastola Askari wa Usalama Barabarani (Trafiki)
Ilikuwa kama mchezo wa kuigiza kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro baada ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, Emmanuel Mkumbo kufikishwa ili apandishwe kizimbani kujibu mashtaka sita, likiwamo la kutishia kuua.
Tukio zima la kumpeleka mahakamani, kumpandisha kizimbani na kumsomea mashtaka kwa muda wa dakika 30 hivi lilitawaliwa na vituko. Kwanza, ni jaribio la kuwaficha wanahabari.
Kabla ya kufikishwa mahakamani, Polisi mkoani Morogoro iliwaarifu wanahabari kuwa ingetoa taarifa kuhusu mkurugenzi huyo lakini saa 4:30 asubuhi wakati Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Ulrich Matei akijiandaa kuzungumza nao, alipigiwa simu akatoka nje ya ukumbi na aliporejea alisema hawezi kutoa taarifa tena na akaondoka.
Waandishi walipofika mahakamani saa 5:00 asubuhi walikuta Kamanda Matei akishuka kwenye gari na alipanda tena akasogea kando kuzungumza na baadhi ya askari wake.
Pili, baada ya hakimu kumaliza kusikiliza kesi hiyo, Mkumbo hakurudishwa mahabusu mahakamani hapo kama ilivyo ada ili kusubiri utaratibu mwingine badala yake mshtakiwa huyo alihamishiwa chumba cha hakimu ambacho hakikuwa na kesi inayoendelea.
Humo ndugu zake walimpelekea koti kubwa jeusi na kofia aina ya pama, hivyo alitoka akiwa tofauti na alivyoingia akiwa na fulana yenye rangi nyeupe, bluu na nyeusi. Baada ya kuvaa alitoka akiwa amezingirwa na polisi, huku ndugu wakiwazuia wanahabari kumpiga picha.
Mashtaka dhidi yake
Mkumbo ambaye ni mkazi wa Tegeta jijini Dar es Salaam alipandishwa kizimbani kujibu mashtaka sita, la kwanza likiwa la kutishia kuua kwa bastola na la pili ni la usalama barabarani lenye makosa matano.
Alisomewa mashtaka hayo na mawakili wa Serikali Sunday Hyera na Edgar Bantulaki. Katika shtaka la kwanza, mbele ya hakimu Agripina Kimaze anadaiwa Oktoba 15, saa 10:30 jioni alitenda kosa la kutishia kuua eneo la Mkambarani, Manispaa ya Morogoro.
Anadaiwa katika shtaka hilo la jinai namba 226 la mwaka 2016, alitishia kumuua kwa bastola askari namba 5057, Koplo Tuti Ndaga wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Morogoro, kinyume na kifungu namba 89 (1),(2),(a) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu namba 16.
Katika shtaka la pili la ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani lenye makosa matano, ilidaiwa kuwa; kwanza, siku na muda huo eneo la Mbuyuni Mkambalani, mshtakiwa alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Prado lenye rangi ya kijivu bila kuwa na leseni.
Pili, ilidaiwa alikuwa akiendesha gari hilo ambalo halikuwa na bima; tatu, alikutwa akiendesha kwa mwendo kasi; na nne, alikataa kupeleka gari Kituo cha Polisi cha Kingoluwira kama alivyoamriwa na askari, WP namba 5392 Sajenti Anna.
Ilidaiwa katika shtaka la tano kwamba, wakati akiendesha alisimamisha gari katikati ya barabara kuu ya Morogoro-Dar es Salaam kwa uzembe, bila uangalifu wala kuzingatia watumiaji wengine wa barabara. Mkurugenzi huyo alikana mashtaka yote yanayomkabili.
Hakimu Kimaze alitoa masharti ya dhamana kwa mshtakiwa kwamba awe na mdhamini mmoja kwa kila shtaka, yaani shtaka la jinai na la usalama barabarani lenye makosa matano, wote wawe wakazi wa Morogoro na mmoja akitakiwa kuweka dhamana ya Sh500,000 kwa kosa la kwanza na Sh1 milioni kwa kosa la pili.
Mshtakiwa alikidhi masharti ya dhamana na kuachiwa huru, huku gari likiendelea kushikiliwa kwenye Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Morogoro.
Hakimu Kimaze aliahirisha shauri hilo hadi Oktoba 31, usikilizwaji wa awali utakapoanza baada ya upande wa mashtaka kudai upelelezi umekamilika.
MPYA:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA THIRD ROUND VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017

,tumedhamiria kuwapa vitu roho inapenda hapa
mjini,Tumeamua kukuwekea list ya vyuo vikuu ambavyo vimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa na joining instructions za kujiunga na vyuo vikuu 2016/2017 THIRD ROUND
CHUO KIKUU NIT (3RD ROUND) >>BONYEZA HAPA<<
CHUO KIKUU ATC ARUSHA (3RD ROUND) >>BONYEZA HAPA<<
CHUO KIKUU MUST-MBEYA (3RD ROUND) >>BONYEZA HAPA<<
CHUO KIKUU AMUCTA (3RD ROUND) >>BONYEZA HAPA<<
CHUO KIKUU MARIAN (3RD ROUND) >>BONYEZA HAPA<<
CHUO KIKUU ST.JOHN DODOMA (3RD ROUND) >>BONYEZA HAPA<<
CHUO KIKUU MOUNT MERU (3RD ROUND) >>BONYEZA HAPA<<











