Serikali ya Tanzania imeagiza kufanyika kwa uchunguzi kuhusu kanda ya
video ilioonyesha kundi moja la walimu likimpiga mwanafunzi.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo tayari amesimamishwa kazi kwa mda kwa
kutochukua hatua hata baada ya kugundua kuhusu kisa hicho ,taarifa ya
serikali imesema.
Raia wa Tanzania katika mitandao ya kijamii walionyesha hasira zao
,wakiitaka serikali kuchukua hatua dhidi ya washambuliaji hao.
Video hiyo ambayo haijakaguliwa inaonyesha mwanafunzi mmoja akipigwa na
kundi la walimu katika kile kinachoonekana kuwa chumba cha wafanyikazi
wa shule.
Katika kanda hiyo ya sekunde 38,takriban watu watano wanaonekana
wakikabiliana na kushambulia mvulana huyo aliyeanguka chini kwa kumpiga
ngumi pamoja na mateke.
Adhabu ya kupigwa viboko ni haramu nchini Tanzania,na kisa hicho cha
hivi karibuni kinatarajiwa kuzua mjadala kuhusu utekelezwaji wa sheria
hiyo katika shule za taifa hilo.
0 comments:
Post a Comment