Leo
October 4, 2016 Naibu waziri wa kilimo mifugo na uvuvi Wiliam Ole Nasha
ameongoza wananchi wa Arusha kwenye misa ya kuaga mwili wa marehemu
Theresia Alex Nguma katika kanisa la mtakatifu Joseph Mfanyakazi Olasiti
jijini Arusha.
Theresia
Alex ni mmoja watafiti waliouawa na wananchi wa kijiji cha Ilinga
mkoani Dodoma baada ya kudhaniwa ni wanyonya damu. Akizungumza kanisani
hapo Waziri Ole Nasha amesema bado serikali inaendelea na uchunguzi
kuhusiana na tukio hilo na watakaobainika watachukuliwa hatua kali za
kisheria.
Imeelezwa
Mpaka kufikia sasa jumla ya watu 45 wamekamatwa na jeshi la polisi
mkoani Dodoma baada ya kuhusishwa na tukio kuwauwa kwa mapanga kisha
kuwachoma moto watafiti wawili na dereva wa chuo cha utafiti wa udongo
na maendeleo ya ardhi cha Seliani Arusha August 1 mwaka huu.
Aidha
Mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqqaro pia ametoa onyo kwa wananchi
wenye tabia ya kuchukua sheria mkononi bila badala ya kufikisha kwenye
vyombo vya dola.
0 comments:
Post a Comment