Propela

aa

million ads

Millionaire  Ads

Tuesday, October 4, 2016

Maamuzi ya Yanga baada ya serikali kuzuia wasitumie uwanja wa Taifa


Ikiwa zimepita siku 2 toka serikali kupitia kwa waziri wa habari, sanaa, utamaduni na michezo Nape Moses Nnauye kutangaza kuufungia uwanja wa Taifa Dar es Salaam kutumia kwa vilabu vya Simba na Yanga, leo October 4 2016 klabu ya Dar es Salaam Young Africans imetangaza kuomba uwanja mbadala watakaotumia kuchezea mechi zao.
Yanga kupitia barua waliyoitoa leo iliyoandikwa na katibu mkuu wao imeomba kuutumia uwanja wa Amaan Zanzibar kama uwanja wao wa nyumbani, katika kipindi hiki ambacho wamezuiwa kutumia uwanja wa Taifa.
Kama utakuwa unakumbuka vizuri waziri Nape alitangaza maamuzi ya kuzizuia timu za Simba na Yanga kwa muda usiojulikana kuutumia uwanja wa Taifa Dar es Salaam kutokana na vurugu na uharibifu uliotokea siku ya mchezo wao wa watani wa jadi uliomalizika kwa sare ya goli 1-1, ila mashabiki walivunja viti na wengine mageti ya kuingilia.

0 comments:

Post a Comment