Baada
ya kufanya gulio kwa wiki iliyopita ambapo simu ziliuzwa kwa bei nafuu
kabisa mtu wangu, Kampuni ya simu za mkononi chini ya Vodacom Tanzania
bado inaendelea kuwawezesha watanzania kumiliki simu imara kwa bei
nafuu kwa kuendelea na gulio katika maduka yao.
Taarifa
iliyotolewa ni kwamba simu ambazo zinapatikana katika maduka hayo ni
pamoja na Smart 7, SmartKicka, Tecno, Itel na Huawei. Mtu wangu ukifika
dukani kwa ajili ya kununua simu mojawapo ya simu hizi utatakiwa kununua
kifurushi tu na baada ya hapo utapatiwa simu ya kijanja na orijino
kulingana na kifurushi alichonunua. Kwa mfano ukinunua kifurushi chenye
dakika 1,400, SMS 10,000 na 5GB za intaneti utapewa Smart 7 BURE kabisa.
Vodacom
wanakujulisha kwamba simu zote hizo zitakuwa zimeunganishwa na intaneti
ambapo mitandao kama Facebook, Twitter, WhatsApp, Snapchat na Instagram
zitakuwa tayari zimeshaingizwa kwenye simu hizo, lakini pia unaweza
kutembelea kurasa za Vodacom Tanzania za mitandao ya kijamii kufahamu
zaidi au duka la Vodacom lililo karibu yako.
0 comments:
Post a Comment