Propela

aa

million ads

Millionaire  Ads

Wednesday, March 15, 2017

Alichojibu Harmonize kuhusu kurudisha ukaribu na mpenzi wake Wolper

Jana March 15 2017 kupitia XXL ya
Clouds FM msanii kutoka WCB
Harmonize amefunguka kuhusu kuhusishwa kuachana na mpenzi wake
Jackline Wolper baada ya kutokuwa na ukaribu nae kwa kipindi kirefu huku kila mmoja akifuta picha za mwenzake kwenye account zao za social.
Harmonize aliulizwa na Mami baby kama ilikuwa kiki au nini baada ya kudaiwa kuachana na Wolper na ukaribu wao kurejea leo wakati anaachia wimbo wake mpya.
“kuna vitu vilitokea tukajikuta hatuko sawa lakini Mungu ndio mwenye kheri tukawa tupo pamoja tukajua kabisa kuwa hiki kitu Jack hakipendi au mimi ila sasa hivi kila kitu kinaenda sawa na Mapenzi yetu sio ya kiki, nafasi yetu kwenye jamii imefanya ionekane kuwa ni kiki nilianza naye nikiwa sina hata gari” – Harmonize.
Harmonize amemtakia kila lenye kheri msanii anayefananishwa naye
Harmorapa nakusema…>>> Ukiona mtu anatumia nafasi yako kuvuma ni jambo la kumshukuru Mungu, sikatai yupo kwenye miahangaiko atatoka, Mungu amjalie najua wote tunatoka kwenye familia za kimaskini ni wakati wake sasa kuonyesha alichojaliwa” :-Hamornize

0 comments:

Post a Comment