Thursday, February 23, 2017
tumejipanga kikamilifu kuimarisha ulinzi na amani katika pambano la watani wa jadi - Jeshi la polisi
Homa ya pambano la watani wa jadi litakalopigwa jumamosi imezidi kupanda huku pande zote mbili zikitamba kuondoka na ushindi na jeshi la polisi likijinasibu kuimarisha ulinzi.
Nelsoni Mandela Madiba alikuwa kinara wa kuandika barua za mapenzi akiwa gerezani,rejea barua yake ya april 27 iliyosheheni majonzi kwenda kwa Winnie ikisema picha yako naipangusa kila asubuhi ninashaka na hofu juu ya kodi ya nyumba na hata chakula kwa watoto,siku moja kablaya pambano la watani hawa nami naadika barua ndefu kwenda kwa wanayanga nikiwambia teke la mwisho la farasi anayekufa huwa na nguvu na wasidaishwe na rangi kwakuwa utamu wa chai sukari.
Tambo zimetamalaki kila pembe ya nchi wayanga wakisema imma faima mnyama haponi simba nao wajibu supu ya mawe i tayari kuwapa yanga zaidi sana jeshi la Polisi nalo lasema litayari kukabiliana na uhalifu.
Homa ya pambano la watani wa jadi litakalopigwa jumamosi inazidi kupanda huku pande zote mbili zikijigamba kuondoka na ushindi wapo Dar es Salaam eneo la kigamboni,wacha nikaskilize wimbo mtoto wacha kupiga mayowe.
0 comments:
Post a Comment