Makamu mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Salum
Shamte akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo
katika ufunguzi mkutano wa wadau wa sekta Binafsi kujadili Tanzania ya
Viwanda ya 2020 Tunayoitaka.
Mkurugenzi Mtendaji wa TPST, Godfrey Sembeye akizungumza na waandishi
wa habari jijini Dar es Salaam leo juu ya maendeleo ya TPSF katika
ukuaji wa uchumi wa viwanda.
Baadhi ya wadau wa Sekta ya viwanda wakiwa katika ufunguzi mkutano wa
wadau wa sekta Binafsi kujadili Tanzania ya Viwanda ya 2020 Tunayoitaka
jijini Dar es Salaam leo.
TANZANIA ni miongoni mwa nchi zinazongoza Afrika kwa kuwa na uchumi unaokuwa kwa kasi ya miujiza.
Hayo ameyasema leo jijini Dar es Salaam, Makamu mwenyekiti wa Taasisi ya
Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Salum Shamte katika ufunguzi mkutano wa
wadau wa sekta Binafsi kujadili Tanzania ya Viwanda ya 2020 Tunayoitaka,
amesema ukuaji wa uchumi katika miongo miwili iliyopita huku pato la
taifa lilikikua kwa wastani wa asilimia 7.0 kwa mwaka katika kipindi cha
kuanzia 2007/2015 lakini lengo la kukua ni asilimia Nane hadi 10 ili
kuweza kutokomeza umasikini uliokidhiri nchini.
Amesema katika kutekeleza na kufanikisha lengo la kitaifa la kuongeza
kipato cha mtanzania mmoja mmoja hadi kufikia Dola za Kimarekani Tatu
(3,000) ifikapo 2025.
Shamte amesema viwanda vina jukumu muhimu katika kusaidia Tanzania
kuinua viwango vya ukuaji wa uchumi katika upatikakanaji wa ajira na
kuboresha maisha ya watu .
Aidha amesema katika fursa ya viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya
kilimo ambapo mazao hayo yanauzwa asilimia kubwa kama mali ghafi.
Shamte amesema kuuzwa kwa mazao ya kilimo kama mali ghafi inachangia
kudororesha kukua kwa sekta ya kilimo ambayo iinakua kwa wastani wa
asilimia 4.2 tu na kufanya umasikini kuendelea kuwepo kwa kiwango cha
juu na kufanya sekta hiyo kuwa na ajira asilimia 67 ya watanzania kwa
sasa.
Amesema sekta binafsi imepewa nafasi kubwa kuchangia maendeleo ya nchi
yetu kutokana Rais Dk.John Pombe Magufuli kuonyesha nia kufanya
majadiliano ya masuala sekta binafsi.
0 comments:
Post a Comment