Propela

aa

million ads

Millionaire  Ads

Thursday, October 6, 2016

Marufuku kujenga maduka kuzunguka maeneo ya shule

Serikali imewaagiza waƙuu wa Mikoa na Wilaya nchini kusimamia na kuanzisha zoezi la kubaini mipaka ya asili ya maeneo yote na kuyapima ili kuhakikisha yanapata hati na kwamba zoezi hilo litekelezwe ndani ya miezi mitatu.

Agizo hilo limetolewa leo na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. George Simbachawene wakati akitoa taarifa ya uvamizi wa maeneo ya shule za msingi, seƙondari na maeneo ya kutolea huduma za afya na masoko yaliyo chini ya ofisi ya Rais TAMISEMI.

Mhe. Simbachawene amesema ni marufuku kujenga vyumba vya biashara kuzunguka shule za msingi, sekonɗari na maeneo ya kutolea huduma za afya, kama chanzo cha mapato kwa sababu kitendo hicho kinasabisha muingiliano usiokubaliana na huduma zinazopaswa kutolewa kwenye maeneo hayo.

Amesema maendeleo yoyote yaliyofanywa na yanayotarajiwa kujengwa kwa ajili ya shughuli hizo hayaruhusiwi, na kwa upande wa shule za msingi na sekondari zilizopo mijini halmashauri zihakikishe zinajenga uzio kuzunguka shule hizo ili kudhibiti muingiliano.

Ametoa wito kwa jamii zinazozunguka maeneo hayo kushirikiana na serikali kwa kutoa taarifa kwa mamlaka za serikali za mitaa juu ya uvamizi huo,kwa kuonyesha alama za asili za mipaka ya maeneo hayo kabla ya kuvamiwa.

Amewataka wananchi waliovamia maeneo hayo ya taasisi hizo waondoke wao wenyewe vinginevyo hatua za kuwaondoa kwa nguvu zitatumika.

Aidha amesena TAMISEMI kwakushirikiana na wizara ya ardhi wameanza taratibu za kutambua haki miliki za ardhi.

0 comments:

Post a Comment