Propela

aa

million ads

Millionaire  Ads

Monday, March 13, 2017

Mwenyekiti wa kitongoji auawa kwa Bastola

Mwenyekiti wa kitongoji cha Kifuru, kijiji cha Ikwiriri, wilayani Rufiji, Hemed Abdallah Njiwa ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake.
Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya Ikwiriri, Iddy Malinda amethibitisha mwili wa mwenyekiti huyo kufikishwa kituoni hapo ukiwa na jeraha kubwa mgongoni lililotokana na risasi aliyopigwa kifuani, upande wa moyo.
Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Juma Njwayo pia amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo na kusema watu wasiojulikana walifika nyumbani kwa mwenyekiti huyo kisha kumpiga risasi na kutokomea kusikojulikana.
Habari zaidi zinadai watu hao baada ya kutekeleza mauaji hayo hawakuchukua kitu chochote kile.

0 comments:

Post a Comment