Propela

aa

million ads

Millionaire  Ads

Wednesday, October 5, 2016

Hali ya uwanja wa ndege wa Songwe Abiria wengi Ndege chache

SHIRIKA la ndege la FastJet limepunguza idadi ya ndege zake kutoka tano zilizokuwepo awali na kubakiwa na ndege mbili tu.
Imedaiwa hatua hiyo imefuatia ujio wa ndege mbili aina ya Bombadier Q400 za serikali zilizokodishwa kwa shirika la Ndege Tanzania (ATCL).
Imeelezwa ujio wa ndege hizo za ATCL umeishtua FastJet hivyo kuona kwamba haitaweza ushindani kutokana na gharama za uendeshaji wa ndege zake kuwa kubwa kuliko zile za ATCL.
Meneja wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe (SIA),Hamisi Amiri,amesema ndege mbili za FastJet zilizopo ndiyo zinazoendelea kufanya safari nchi nzima, kutoka Dar es Salaam kwenda mikoani na nyingine inakwenda nchi jirani za Zambia, Malawi, Zimbabwe na Afrika Kusini.
“Kinachofanyika sasa ni kuwa hapa Mbeya kulikuwa na ndege mbili za FastJet  kwa siku sasa hivi imebakia ndege moja, hivyo abiria wa ndege ya asubuhi na jioni wanaunganishwa pamoja na kupandishwa ndege moja” alisema Amiri.
Amiri alisema awali ndege ya asubuhi ya FastJet, ilikuwa inaondoka uwanjani hapo saa 3:00asubuhi, lakini kuanzia Ijumaa ya wiki iliyopita ndiyo tatizo limeanza, ambapo ndege hiyo ilikuwa inaondoka saa 5:00asubuhi, saa 6:00 mchana na siku nyingine saa 7:00 mchana.
Kwa mujibu wa Amiri, ili kuwaunganisha abiria wake FastJet wamekuwa wanawapigia simu abiria, na wale ambao wanakuwa hawajapatikana, huwa wanafika uwanjani hapo na kukuta kukiwa hakuna ndege, hali inayoleta usumbufu kwa abiria.
“Hivi sasa asubihi abiria wanaokuja hapa SIA wanakuwa zaidi ya 250 hadi 300, wote wanataka kusafiri na ndege moja yenye uwezo wa kubeba abiria 150.Wanachofanya FastJet wanatumia ule mtindo wa abiria aliyewahi kufika uwanjani ndiyo anakuwa wa kwanza kuondoka” alisema Amiri.
Aliongeza hivi sasa abiria wamekuwa wanafika uwanjani hapo kuanzia saa11:00 alfajiri, hivyo waliowahi ndiyo huwa wanahesabiwa hadi abiria wa 150, hao ndio wanaoondoka hali inayopelekea asubuhi kunakuwa na foleni ndefu SIA.
Amiri alisema hivyo hata kama abiria ilikuwa ni siku yake ya kusafiri, na alikuwa hana taarifa juu ya uwepo wa abiria wengi, anachelewa kufika uwanjani hapo, na akifika anakutana na foleni ndefu, hivyo anakuwa yupo nje ya abiria wanaotakiwa kusafiri.
Meneja wa SIA Amiri  alisema hali hiyo imekuwa inawachanganya abiria wengi, ambapo juzi abiria walitaka kuvunja milango uwanjani, wakidai kama vipi watapigana kwenye ndege ama watadandia mabawa ya ndege, hali ambayo imekuwa inapelekea usumbufu mkubwa.
Aliongeza hivyo kutoka Ijumaa hadi jana Oktoba 3, mwaka huu hali ilikuwa mbaya, lakini Oktoba 4, mwaka huu kidogo hali imekuwa nzuri kwani abiria wote wameweza kusafiri, na inaonyesha wengi wameamua kusafiri kwa njia nyingine ikiwemo usafiri wa mabasi.
Aliongeza hatua hiyo inatokana na kishindo cha ujio wa ndege mbili za ATCL, ambapo Fast Jet wamekuta gharama ya kuziendesha ndege zao ni kubwa, hivyo wamekuta hawataweza kushindana na ATCL hivyo nao wameamua kuzirudisha ndege zao kubwa ili wanunue ndege ndogo.
Uchunguzi uliofanywa na Muungwana blog wanjani hapo,unaonyesha FastJet walikuwa wanafikiri serikali haitaweza kununua ndege mbili kama ilivyokuwa imeahidi, hali inayoonyesha walikuwa hawajajipanga vizuri.

0 comments:

Post a Comment