October 3, 2016 Mtu wangu wa nguvu nakusogezea taarifa ya Benki ya Dunia kuhusu kupungua kwa idadi kubwa ya watu masikini duniani licha ya ongezeko la idadi ya watu ulimwenguni.
Kwa
mujibu wa Benki ya Dunia ripoti inasema kuwa, idadi ya watu masikini
sana imepungua kwa zaidi ya watu milioni 100 licha ya kwamba uchumi wa
dunia unakuwa kwa kusua sua.
Kwa mujibu
wa takwimu za hivi karibuni kutoka Benki ya Dunia, mwaka 2013 karibu
watu milioni 767 walikuwa wanaishi kwa pato la dola 1.90 kwa siku wakati
mwaka 2012 idadi ya watu masikini sana ilikuwa ni milioni 881 kote
ulimwenguni.
Ripoti
hiyo pia imeonesha kuwa, mwaka 2013 idadi ya watu masikini
zaidi ilipungua kwa karibu watu bilioni moja na milioni mia moja
ikilinganishwa na mwaka 1990 licha ya idadi ya watu kuongezeka duniani
huku ikieleza kuongezeka kwa misaada kwa watu masikini duniani.
Takwimu
hizo zinaonesha kuwa, dunia imekaribia kufikia malengo yaliyokusudiwa na
Umoja wa Mataifa ya kupunguza umaskini kwa kiwango kikubwa ifikapo
mwaka 2030.
0 comments:
Post a Comment