Propela

aa

million ads

Millionaire  Ads

Friday, March 17, 2017

Maharamia Wa Kisomali Waiachia Huru Meli

Maharamia waiachia huru Meli
Maharamia wa Kisomali wameiachia huru meli ya mafuta waliyokuwa wameikamata kwenye pemba ya Afrika siku ya Jumatatu bila ya kulipwa fedha.
Maafisa nchini Somalia wamesema wafanyakazi saba wa meli hiyo raia wa Sri Lanka waliachiwa pia bila ya kudhuriwa.
Meli hiyo ilikamatwa katika eneo la pwani ya Puntland siku ya Jumatatu, ikiwa ni mara ya kwanza katika eneo hilo katika kipindi cha miaka mitano.
Maharamia hao waliiachia meli hiyo baada ya mazungumzo yao na askari wanamaji wa Puntland.

0 comments:

Post a Comment