Propela

aa

million ads

Millionaire  Ads

Friday, October 7, 2016

AyoTV Tecno Phantom 6 kuanza kuuzwa, haya ni mambo ya kuyafahamu

Baada ya simu ya Tecno Phantom 6 na Phantom 6 plus kuzinduliwa usiku wa September 26 2016 huko Dubai kwenye jengo refu zaidi duniani, Burj Khalifa, October 8 2016 ndio siku pekee ya wewe mtu wangu kuweza kumiliki kifaa hicho kipya cha phantom 6 kwa kuinunua kwa mara ya kwanza hapa Tanzania katika viwanja vya City Mall Posta jijini Dar es Salaam. Simu hizo za Phantom 6 na phantom 6 plus zitakua na 32GB ROM, 3GB RAM na kamera mbili za nyuma zenye 13MP na 5MP, muonekano wa kuvutia pamoja na uwezo wake wa ajabu wa kuingiza chaji kwa haraka zaidi na kutunza chaji kwa muda mrefu. Vile vile mtu wangu ukiinunua Phantom 6 katika viwanja hivyo basi utapata nafasi ya kujishindia zawadi kem kem. Hizi ndizo zawadi ambazo unaweza kujishindia endapo utanunua phantom 6 kwa siku hiyo Kupata zawadi za TECNO kama T-Shirt, T-Band, begi na Selfie stick Kushiriki katika bahati nasibu na kupata nafasi ya kujishindia tiketi za kuangalia filamu, Winpad, Power bank na Kamera ya kupaa ( Drone) Kushiriki katika ulengaji wa puto na kupata nafasi ya kushinda zawadi mbalimbali droo Ndege hii ya kupaa itazawadiwa kwa mteja mmojawapo miongoni mwa wateja watakaojitokeza tarehe 8 Oktoba katika mauzo ya kwanza ya Tecno Phantom 6. Unaweza kupata taarifa zaidi kwa kutembelea kurasa za mitandao ya kijamii ya Tecno. Facebook: https://www.facebook.com/TECNOMobileTanzania/?fref=ts Instagram: https://www.instagram.com/tecnomobiletanzania/ Twitter: https://twitter.com/TECNOMobileTZ

0 comments:

Post a Comment