Thursday, February 2, 2017
Waziri Kairuki Azindua Rasmi, Ofisi Ya Rais –Utumishi Na Utawala Bora Iliyopo Makao Makuu Ya Nchi Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akikata utepe kuzindua rasmi ofisi yake iliyopo Makao Makuu ya Nchi Dodoma. Wanaoshuhudia ni watumishi wa ofisi hiyo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akizungumza na Vyombo vya Habari kabla ya kuzindua rasmi utoaji wa huduma wa ofisi yake iliyopo Makao Makuu ya Nchi Dodoma. Wengine ni baadhi ya Watumishi wa ofisi hiyo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akijionea moja ya shubaka linalotumika kutunzia majalada katika masijala ya ofisi yake, mara baada ya kuzindua utoaji wa huduma wa ofisi hiyo iliyopo Makao Makuu ya Nchi Dodoma. Wanaoshuhudia ni baadhi ya watumishi wa ofisi hiyo na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Prof. Idris Kikula.



0 comments:
Post a Comment