Propela

aa

million ads

Millionaire  Ads

Thursday, January 12, 2017

Aliyenusurika ajali boti arukwa akili

MMOJA wa manusura 33 wa ajali ya boti iliyozama Bahari ya Hindi na kusababisha vifo vya watu 13, amebainika kurukwa na akili na matabibu wa Hospitali ya Rufaa ya Tanga wanaomtibu. Image Juzi Alfajiri, boti ya Burudan, maarufu Sayari, yenye namba za usajili MV 25512, mali ya Suleiman Vuai, mkazi wa Pemba, ilizama karibu na Kisiwa cha Jambe ilipokuwa inatoka bandari bubu ya Sahare jijini Tanga kwenda Pemba ikiwa na shehena ya chakula, bia na abiria zaidi ya 40. Katika ajali hiyo, watoto sita walikuwa miongoni mwa watu 12 waliopoteza maisha huku 33 wakiokolewa na wavuvi wakiwa hai na kukimbizwa kwenye hospitali hiyo, maarufu Bombo. Hata hivyo, jana jioni Kaimu Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Dk. Goodluck Mbwilo, aliambia Nipashe jijini humu kuwa majira ya saa 10 alasiri walipokea maiti ya mtoto mwenye umri kati ya miaka mitano na sita ikiwa imeharibika. Hadi jana saa 9:38 alasiri, manusura 32 walikuwa wameruhusiwa kuondoka hospitalini hapo huku msichana mmoja mwenye umri wa miaka 12 akishindwa kuruhusiwa kutokana na kurukwa akili. Msichana huyo (jina tunalihifadhi) amebainika kurukwa na akili kutokana na ajali hiyo ambacho taarifa za awali zinadai ni mawimbi makali yaliyopiga boti hiyo na kusababisha maji kuingia ndani.

0 comments:

Post a Comment