Propela

aa

million ads

Millionaire  Ads

Saturday, December 24, 2016

Sam Allardyce ateuliwa kuwa kocha mpya wa Crystal Palace

Klabu ya Crystal Palace ambayo inashriki ligi kuu ya Uingereza, hatimaye imemtangaza Sam Allardyce kuwa kocha mpya wa klabu hiyo baada ya kumfuta kazi kocha Alan Pardew wakati ambapo klabu hiyo iko katika nafasi ya 17 katika ligi hiyo. Sam Allardyce amesaini mkataba wa miaka miwili na nusu, Big Sam ambaye aliingia matatani na chama cha soka nchini Uingereza (FA) na kutumuliwa kuwa kocha wa timu ya taifa ya Uingereza, baada ya kuwaeleza waandishi wa habari wa gazeti la Daily Telegraph waliojifanya wafanyabiashara kuwa ni rahisi kuizunguka sheria ya chama cha soka nchini Uingereza (FA).

0 comments:

Post a Comment